Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wanawake wapewa somo la unyonyeshaji
Habari Mchanganyiko

Wanawake wapewa somo la unyonyeshaji

Mama akinyonyesha mtoto
Spread the love

WANAWAKE wamehimizwa kunyonyesha watoto kwa kipindi kinachoshauriwa kitaalamu ili kuwaepusha na madhara ya utapiamlo na udumavu wa akili, anaadika Mwandishi Wetu.

Mratibu wa Jinsia na Lishe wa Shirika la Taha, Salome Stephen alisema hayo wakati akizungumza na wajumbe wa Kamati za Lishe za Wilaya ya Babati Mjini na Babati Vijijini ili kufahamu changamoto wanazokabiliana nazo.

“Jamii inatakiwa kuwa makini zile siku 1000 tokea ujauzito umeingia kumlea vizuri mtoto ambazo ni sawa na ile miezi tisa ya ujauzito na miaka miwili baada ya kuzaliwa mtoto,’’ amesema

Mtaalamu huyo wa masuala ya lishe alisema iwapo wazazi wakikosa hasa wakina mama wakashindwa kuwanyonyesha watoto kwa kipindi cha miezi sita mfululizo na wakawapa vyakula vingine kama vile uji ndio watakuwa wamearibu mtoto au watoto kiakiri.

“Kama wazazi wakikosea kumpa mtoto vyakula vya kumjenga kiakiri ndani ya siku 1000 hakuna tena wakati wa kuweza kurekebisha na kuondoa makosa uliyoyafanya hivyo wanatakiwa kua makini kipindi hicho,’’ alisisitiza.

Aidha, aliwataka wanawake kuwanyonyesha watoto wao kikamirifu kutwa mara kumi ila isipungue ndipo wanaweza wakawaepusha na utapiamlo na kuwaandalia mazingira rafiki ya kuja kufanya vizuri watakapoanza masomo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!