Wednesday , 24 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wanawake Babati walalamikia kuswekwa Rumande
Habari Mchanganyiko

Wanawake Babati walalamikia kuswekwa Rumande

Spread the love

WANAWAKE wanaofanya biashara ya kuuza samaki  maeneo ya  stendi  kuu ya mabasi mjini hapa wameilalamikia Halmashauri ya Mji wa Babati kuwaondoa  kwa nguvu na kuwasweka rumande bila kuwaandalia mazingira mengine, anaandika Mwandishi Wetu.

Malalamiko hayo waliyatoa wakati wakizungumza na wakiwa  maeneo ya  zima moto  ilipo ofisi ya kata walipokuwa wameswekwa rumande ya kata kabla ya kuwafikisha kituo cha polisi cha Babati.

“Sisi tuna uwezo mdogo wa kifedha na mitaji yetu haizidi  Sh 20,000 wakituondoa hapa tutaenda wapi maana kule wanakolazimisha tuende  hamna wateja  kwa kua sisi tunawauzia wasafiri,’’alisema Janeth Edison.

Wachuuzi hao walisema wanashindwa kukubaliana na  matakwa ya Halmashauri kwa kuwa  eneo wanaloambiwa kupewa sokoni ni nyuma sana ambako hawawezi kupata wateja.

Aidha,  wanasema baadhi ya watumishi wa Halmashauri wamewageuza kitega uchumi chao kwa kua wanawatoza faini  ya Sh 90,000 lakini wakati wakiandika risiti wanaandika wamelipia 50000 suala ambalo walidai linawaumiza.

“Tulipoenda kwa Kaimu Mkurugenzi, Bashir  Mhoja, alituambia  hawatatutafutia eneo jingine  tulipomfuata ofisini  badala yake alisema watatukamata na kututoza faini  au kutufikisha mahakamani,’’ alisema Zakia  Amani.

Naye Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Babati Mjini, Fauswali  Hamadi, alisema  ni vizuri tatizo hilo likamalizwa kwa busara.

Alisema Rais John Magufuli alishatangaza mara kwa mara kwamba wafanyabiashara ndogondogo (wamachinga) waachwe wakiendelea na bishashara zao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

error: Content is protected !!