Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Maisha Afya Wanaume wabanwa likizo ya uzazi
Afya

Wanaume wabanwa likizo ya uzazi

Spread the love

WANAUME wanaopewa likizo ya uzazi, wameshauriwa kutumia vizuri kwa kumsaidia mama aliyejifungua, na kwamba ni kwa mujibu wa sheria ya kazi na ajira ya mwaka 2004. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Kauli hiyo imetolewa jijini Dodoma leo tarehe 2 Agosti 2019 na Ummy Mwalimu, Waziri wa afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto mbele ya vyombo vya habari kuhusu maashimisho ya wiki ya unyonyeshaji duniani.

Akitoa tamko la serikali kuhusu kuanza kwa wiki ya unyonyeshaji Waziri Mwalimu amesema, likizo ya wanaume sio kwa ajili ya kwenda kustarehe kwenye Bar, bali ni kwa ajili ya kutoa usaidizi kisaikolojia kwa wanawake waliojifungua.

“Tunapokea malalamiko kwamba baadhi ya wanaume wanaopewa likizo ya uzazi, huwa hawaonekani kabisa nyumbani na wengine hutumia siku hizo tano kwa ajili ya kustarehe na wanawake wengine, hii haiko sawa kisheria,” amesema.

Mbali na hayo amesema, kimsingi likizo hiyo ni maalumu kwa ajili ya baba kumsaidia mama majukumu ya kifamilia anapokuwa amejifungua, na si vinginevyo.

“Wizara yetu itafanya utafiti kama kweli likizo hii ina manufaa, na kama tukijiridhisha kuwa haina manufaa lazima tuifute,” amesisitiza.

Pamoja na hayo amewataka waajiri kuzingatia sheria ya ajira na mahusiano kazini, kwa kumpatia haki ya kunyonyesha mama aliyejifungua.

“Wanawake wanaonyimwa haki hii, watoe taarifa kwa maofisa kazi katika halmashauri zao kwasababu msipojitokeza kudai haki yenu, sisi hayutaweza kujua,” amesisitiza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

Marekani kuipa Tanzania bilioni 980 kudhibiti VVU, UKIMWI

Spread the loveSERIKALI ya Tanzania inatarajiwa kupewa msaada wa fedha kiasi cha...

AfyaHabari Mchanganyiko

Wanavijiji wajenga zahanati kukwepa umbali mrefu kupata huduma

Spread the loveWANAVIJIJI wa Kata ya  Musanja Jimbo la Musoma Vijijini, mkoani...

AfyaTangulizi

Wanasayansi wagundua teknolojia ya kunyofoa VVU kutoka kwenye seli

Spread the loveTIMU ya wanasayansi kutoka Chuo Kikuu cha Amsterdam cha nchini...

Afya

Wananchi 530,000 kufaidika na ujenzi wa hospitali ya bil. 1.8

Spread the love  SERIKALI imetoa Sh 1.8 bilioni kwa ajili ya ujenzi...

error: Content is protected !!