Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Wanaoongoza kanda Chadema hawa hapa 
Habari za Siasa

Wanaoongoza kanda Chadema hawa hapa 

Lazaro Nyalandu, Mwenyekiti wa Kanda ya Kati Chadema
Spread the love

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimewatangaza viongozi wake 29 wa kanda, waliochaguliwa katika chaguzi zilizofanyika kuanzia tarehe 28 Novemba hadi Desemba Mosi mwaka huu. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Viongozi hao, wametangazwa leo tarehe 3 Desemba 2019 na Tumaini Makene, Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano Chadema.

Viongozi wa Kanda ya Serengeti ni Esther Matiko, mwenyekiti wa kanda hiyo, wakati makamu wake akiwa Gimbi Massaba, huku mweka hazina akiwa Bernard Makoye.

Ezekiel Wenje amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Kanda ya Victoria, ambapo msaidizi wake ni Sylivester Makanyaga na mweka hazina ni Upendo Peneza.

Kanda ya Pemba inaongozwa na Hafidh Ali Saleh aliyechaguliwa kuwa mwenyekiti wa kanda hiyo, Time Ali Suleiman, Makamu Mwenyekiti na Ali Khamis Ali, Mweka Hazina.

Said Mzee Said amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Kanda ya Unguja, wakati makamu wake ni Hassan Abeld na Asiata Said Abubakari, Mweka Hazina.

Kanda ya Kusini Mwenyekiti wake ni Seleman Mathew, Makamu Mwenyekiti ni Salum Barwan na Mweka Hazina, Mario Milllinga.

Kanda ya Nyasa itaongozwa na Mchungaji Peter Msigwa (Mwenyekiti), akisaidiwa na Joseph China (Makamu Mwenyekiti) na Mweka Hazina ni Aidan Khenan.

Lazaro Nyalandu, Mwenyekiti wa Kanda ya Kati, wakati Makamu Mwenyekiti akiwa Aisha Luja, na Mweka Hazina ni Devotha Minja.

Kanda ya Magharibi viongozi wakee ni Gaston Garubindi (Mwenyekiti), Masanja Musa (Makamu Mwenyekiti) na Aidan Ndowa (Mweka Hazina).

Hata hivyo, Kanda ya Pwani haina mwenyekiti kufuatia aliyekuwa mgombea pekee wa nafasi hiyo Fredrick Sumaye kushindwa katika kura za ndio au hapana, kwenye uchaguzi uliofanyika tarehe 28 Novemba mwaka huu.

Hivyo, uchaguzi wa nafasi ya mwenyekiti wa kanda hiyo utarudiwa. Aliyechaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti ni Baraka Mwago na Mweka Hazina ni Dk. Michael Mtaly.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Mwakyembe : Zanzibar waliongoza kutaka Serikali 2 za muungano

Spread the love  MWANASIASA mkongwe nchini, Dk. Harrison Mwakyembe, amesema mjadala wa...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

error: Content is protected !!