Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Wananchi watakiwa kutumia maharage ya SUA
Habari Mchanganyiko

Wananchi watakiwa kutumia maharage ya SUA

Zao la maharage
Spread the love

JAMII imeshauriwa kubadilika na kula maharage ya SUA Karanga ambayo yanatengenezwa na watafiti kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) huku yakiwa hayana gesi na yenye protini zaidi zinazopatikana katika nyama kwa afya. Anaripoti Christina Haule, Morogoro … (endelea).

Meneja Utafiti wa Maharage hayo Profesa Paulo Kusolwa alisema hayo wakati wa maonesho ya wakulima 88 kanda ya Mashariki yaliyofanyika kwenye uwanja wa Mwalimu Julius Nyerere ambapo alisema, maharage hayo ni tofauti na maharage mengine kwani yana uwezo wa kuliwa hata na mtu mwenye vidonda vya tumbo na asipate madhara.

Prof. Kusolwa alisema, waliamua kufanya utafiti na kuboresha maharage yanayotumika masokoni kwa kuweka vinasaba au viini vya uvumilivu wa magonjwa na wadudu ili kumsaidia mlaji na mkulima zaidi.

Alisema, jamii ya Maharage ilikuwa na tabia ya kutoa wadudu muda mfupi baada ya kuvunwa na kuzalisha mazao kidogo na kwamba maharage hayo ambayo yanazalisha zaidi hayatoi wadudu wala hayaliwi na wadudu baada ya kuvunwa .

Hivyo aliwashauri wakulima kutumia mbegu za maharage hayo ambazo zinapatikana kwa wingi SUA ili kuweza kuongeza uzalishaji wa mbegu na kumfanya mlaji kupata chakula hicho kwa afya.

Alisema, mpaka sasa wana aina 6 za mbegu za maharage ambazo wanaendelea kuzifanyia tafiti kwa ufadhili wa Shirika la Msaada la Marekani lijulikanalo kama The Mcnight Foundation lengo likiwa ni kupata mbegu bora itakayoendana na hali ya hewa ya aina zote na kumnufaisha mlaji na mkulima.

Hata hivyo Prof. Kusolwa alisema, ni vema ukawepo msukumo wa kisera wa kuboresha lishe kwa watoto mashuleni, wafungwa magerezani na wagonjwa hospitalini ili kuifanya mbegu hiyo yenye lishe kuweza kupata soko na kuingia kwa wingi katika jamii tofauti na ilivyo kwa sasa.

Alisema licha ya mbegu hiyo kuwa bora lakini bado haijapata masoko ya uhakika na kwamba mpaka sasa wana hifadhi ya Tani 30 ndani jambo ambalo huifanya kuendelea kubaki kwenye makabati na hivyo kutoleta maana ya utafiti.

Alisema SUA Karanga ina uwezo wa kuzalisha kg 25-30 kwa kg 1 ya mbegu ambapo pia huweza kupatia mkulima gunia 25 za maharage hayo baada ya kuvuna hekari 1 ya maharage hayo.

Hivyo aliomba wakulima waipokee mbegu hiyo kwa mikono miwili kufuatia kuweza kuongeza chakula kilichoboreshwa sambamba na kuwaongezea kipato.

Naye Mkulima Mzee Flaiton Mlozi wa kijiji cha Nambala – Mbozi mkoani Songwe alisema mbegu hiyo imeweza kuwa na manufaa kwake kufuatia kuwa na mavuno mengi licha ya kukabiliwa na changamoto ya soko.

Alisema awali alikuwa akilima shamba la nusu heka lakini amelazimika kuongeza ukubwa wa shamba na kulima shamba la heka mbili kutokana na kuwa na mavuno mengi na mbegu nyingi kwa sasa.

Hivyo aliiomba Serikali kuingilia kati na kuona umuhimu wa kuwatafutia masoko ili waweze kuuza tofauti na kuwasubiri SUA kwenda kununua maharage hayo kwao huku wao na wakiwa na nia ya kuuza mapema kwa ajili ya kukidhi mahitaji yao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

DAWASA waanza utekelezaji agizo la Samia

Spread the loveMamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam...

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

error: Content is protected !!