Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya Wananchi watakiwa kupima afya zao mara kwa mara
Afya

Wananchi watakiwa kupima afya zao mara kwa mara

Dk. Faustin Ndungulile
Spread the love

IKIWA leo tarehe 4 Februari 2019 dunia inaadhimisha siku ya saratani, serikali imeendelea kusisitiza wananchi kupima afya zao ili kukabiliana na ugonjwa huo. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Wito huo umetolewa leo tarehe 4 Februari 2019 bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Faustine Ndugulie.

Dk. Ndugulile ameeleza kuwa, watanzania wengi wenye ugonjwa wa saratani huchelewa kufika hospitali kwa ajili ya matibabu kitendo kinachopelekea kukosa tiba kwa wakati na kufariki dunia.

Amesema, takribani watu 55,000 hupata ugonjwa wa saratani kila mwaka, ambapo wanaowahi kufika hospitali kwa ajili ya vipimo na matibabu ni asimilia 25 pekee, huku asilimia 70 wakifika katika hatua za mwisho.

“ Watu 55,000 hupata saratani kwa mwaka, asilimia 25 wanawahi kufika, asilimia 70 wanafika wakiwa wamechelewa. Tunawataka Watanzania kujitokeza kwa wingi sababu kupima ni bure,” amesema Dk. Ndugulile.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari za Siasa

Serikali yasaka watumishi afya ngazi ya jamii 8,900

Spread the loveSERIKALI imeanza utekelezaji wa mpango jumuishi wa wahudumu wa afya...

AfyaHabari za SiasaTangulizi

Bima ya afya kwa wote kuanza Aprili, wajane kicheko

Spread the loveSHERIA ya Bima ya Afya kwa Wote, inatarajiwa kuanza kutumika...

AfyaHabari Mchanganyiko

Marekani kuipa Tanzania bilioni 980 kudhibiti VVU, UKIMWI

Spread the loveSERIKALI ya Tanzania inatarajiwa kupewa msaada wa fedha kiasi cha...

AfyaHabari Mchanganyiko

Wanavijiji wajenga zahanati kukwepa umbali mrefu kupata huduma

Spread the loveWANAVIJIJI wa Kata ya  Musanja Jimbo la Musoma Vijijini, mkoani...

error: Content is protected !!