Thursday , 18 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wananchi wahimizwa kuwekeza kwenye hisa
Habari Mchanganyiko

Wananchi wahimizwa kuwekeza kwenye hisa

Mkurugenzi wa Bodi ya TCCIA, Donald Kamori
Spread the love

WANANACHI wametakiwa kuhudhuria semina zinahusua uwekezaji wa hisa ili wapate elimu itakayowasaidia kupata ufahamu kwa undani kuhusu biashara hiyo endelevu, anaandika Angel Willium.

Rai hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Uwekezaji ya TCCIA Investment, Arphaxad Masumbu wakati wa kuanzimisha miaka 12 ya wanahisa nchini yaliyofanyika jijini Dar es Salaam.

Masumbu amesema wanachangamoto ya kutokuwa na watu wengi katika ununuaji wa hisa, hilo linatokana na wananchi kutokuwa na elimu juu ya biashara hiyo yan uwekezaji.

“Mikoani kumekuwa na mwitikio mdogo, wakushiriki semina za elimu kwa wananchi, hivyo tunaingia gharama kubwa kuandaa mikutano, watu hawajui kwamba biashara ya kununua na kuuza hisa ni endelevu kwani usipofaidika wewe basi itamsaidia mtoto wako,” amesema Masumbu.

Naye Mkurugenzi wa bodi ya TCCIA, Donald Kamori amesema wameimalisha mtaji wao ambao kwa sasa umefikia Tsh. 1.28 bilioni kutoka 1.9 bilioni, fedha hizo wamewekeza kwenye makapuni mbalimbali kama bank NMB na mengineyo.

TCCI Investment imeazimisha miaka 12 ya tangu kuanzishwa mwaka 2005, mwaka jana waliweza kutekeleza majukumu ya kusimamia zoezi la kuthaminisha mali za kampuni.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

Habari Mchanganyiko

Serikali yatoa ajira watumishi 46,000, yatangaza utaratibu mpya kuajiri

Spread the loveSERIKALI imetangaza nafasi za ajira za watumishi wa umma 46,000...

error: Content is protected !!