Tuesday , 19 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Wananchi wa Dar poleni na mafuriko
Habari za SiasaTangulizi

Wananchi wa Dar poleni na mafuriko

Spread the love

MVUA kubwa zinazoendelea kunyesha jijini Dar es Salaam, zimesababisha madhara makubwa katika baadhi ya maeneo, ikiwamo watu kupoteza maisha na kutokuwa na makazi.

Hata hivyo, kumekuwapo na madai kuwa serikali imetimiza majumu yake kwa kuwataka wananchi waishio mabondeni kuhama katika maeneo wanayoishi.

Aidha, serikali na baadhi ya wanasiasa wamekuwa wakiwatuhumu wananchi kuwa wamekuwa wakaidi mno wa kutuoondoka kwa maeneo yao.

Kumekuwapo na hata madai kuwa serikali imetoa viwanja kadhaa pembezoni mwa jiji kwa wananchi, lakini wananchi hawavitaki viwanja hivyo.

Si hivyo tu: Kumekuwapo na maneno kuwa jiji la Dar es Salaam, limejaa na halina tena nafasi ya kupokea watu wengine zaidi.

Napenda kueleza yafuatayo:

Dar es Salaam halijaja. Iimejazwa kutokana na mipango mibovu ya serikali ya CCM. Iimejezwa kwa sababu ya mchoko wa mawazo wa viongozi walioko madarakani.

Iimejezwa kutokana na ubinafsi, upendeleo na undumilakuwili wa CCM na serikali yake. Basi.

Nenda pale bonde la Msimbazi ambako maji yote yanayotoka Tabata, Pugu, Kisukulu, Kigogo, Mabibo, Kimara, Buguruni na maeneo mengine ya jiji, ukajionee jinsi maji yalivyozuia na kuta za viwanda zilizojengwa pembezoni mwa mikondo ya maji kwa ruhusa ya serikali.

Nenda Bonde la Msimbazi, eneo la Sukita ukaone jinsi lilivyobinafishwa na CCM kwa muwekezaji feki na ambaye amejenga ukuta unaozuia maji kutililika kuelekea baharini.

Angalia wananchi wanaoteseka kutokana na uroho huu wa fedha wa viongozi wao.

Hatua ya ujenzi huo, imeababisha mafuriko na uhalibifu mkubwa wa nyumba za watu.

Wananchi wamepigia kelele sana mipango mibovu ya ujenzi inayosimamiwa na kuratibiwa na serikali.

Hata hivyo, hakuna hatua zinazochukuliwa kwa kuwa baadhi ya wafanyabiashara waliojenga katika maeneo hayo, ama ni wafadhili wa moja kwa moja wa CCM; na au baadhi ya viongozi wake.

Kwa muktadha huo, anayepaswa kulaumiwa katika hili, siyo wananchi. Ni serikali.

Saed Kubenea,

Mbunge wa Ubungo

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Zanzibar mbioni kuanza uchimbaji mafuta na gesi baharini

Spread the loveSERIKALI ya Zanzibar, imekamilisha mchakato wa uchimbaji wa mafuta na...

Habari za Siasa

Wizara ya afya yataja mafanikio 10 miaka mitatu Samia madarakani

Spread the loveWIZARA ya Afya imetaja mafanikio 10 iliyoyapata ndani ya miaka...

Habari za Siasa

Mbozi walilia kuwa manispaa, majimbo 3

Spread the loveHALMASHAURI ya wilaya ya Mbozi mkoani Songwe imeeleza dhamira yake...

Habari za Siasa

Wabunge waitaka TPDC kuongeza kasi ya kuunganisha wateja gesi asilia

Spread the love  KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini...

error: Content is protected !!