WANAFUNZI kadhaa katika Shule ya Msingi Seliani iliyoko wilayani Arusha wanadaiwa kutumbukia katika shimo la choo cha shule hiyo mchana huu. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).
Taarifa za tukio hilo zimesambaa mchana wa leo tarehe 26 Oktoba 2018 katika mitandao ya kijamii.
Kufuatia tukio hilo, Mtandao huu ulimtafuta kwa njia ya simu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, SACP Ramadhan Ng’azi ili kupata uthibitisho wa tukio hilo.
SACP Ng’azi ameuambia mtandao huu kuwa, hana taarifa za tukio hilo kwa muda huu, na kwamba anafuatilia tukio hilo kisha baadae atatoa taarifa sahihi.
Leave a comment