Wednesday , 24 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Wanafunzi elimu ya juu wapata mtetezi
Habari za Siasa

Wanafunzi elimu ya juu wapata mtetezi

Waziri Kivuli Wizara Ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na Mbunge wa Viti Maalum Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Suzan Lyimo
Spread the love

Waziri Kivuli Wizara Ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na Mbunge wa Viti Maalum Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Suzan Lyimo, amesema muongozo au masharti  ya kuomba mkopo uliotolewa na Bodi ya Mkopo wa Elimu ya Juu (HELSB), zinakasoro mbalimbali zinazowanyima Vijana wakitanzania uhuru wa kupata Elimu, anaandika Irene David.

“Elimu au kuelimika ni kibali cha maisha ya baadae kwa kuwa kesho ni kwa ajili ya wale walioiandaa leo,” sisi leo hatumwandalii huyu kijana elimu bora halafu umtegemee vipi kuijenga nchi yake kesho, amesema Lyimo.

Lyimo amesema hayo leo wakati akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi zake zilizopo makao makuu ya Chadema amesema masharti hayo ni kama, Awe amemaliza kidato cha sita au awe na sifa linganish kama Diploma ndani ya miaka mitatu, waombaji ambao wazazi wao ni Wakurugenzi au Mameneja waandamizi hawatarajiwi kuomba na waombaji ambao wazazi wao ni viongozi wa umma au kisiasa ambao wanatajwa na sheria ya maadili ya viongozi wa umma.

Amebainisha kwamba katika sifa hizo zinazidi kuimarisha dhana ya ubaguzi na matabaka katika utoaji wa elimu nchini pia hazina uhalisia ya utekelezaji chanya kwa mazingira ya nchi na utekelezaji wake zipo kinyume na katiba.

Lyimo ameitaka serikali kutafuta njia mbadala au vyanzo vya kugharamia elimu ya juu mfano mabenki kwa riba nafuu na kuitaka tume ya Haki za Binadamu kuingilia kati suala hili .

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

Habari za SiasaTangulizi

Shibuda amlima waraka mzito Bulembo

Spread the loveMKONGWE wa siasa nchini, John Shibuda amemshukia kada maarufu wa...

error: Content is protected !!