Tuesday , 16 April 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Wanafunzi 215 wafutiwa matokeo, 252… 
Elimu

Wanafunzi 215 wafutiwa matokeo, 252… 

Katibu Mtendaji wa Necta, Dk. Charles Msonde
Spread the love

BARAZA Mitihani la Tanzania (Necta), limefuta matokeo yote ya watahiniwa 215, waliofanya udanganyifu katika mitihani yao ya Taifa mwaka 2020. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Hayo yamesemwa leo Ijumaa tarehe 15 Januari 2021, na Katibu Mtendaji wa Necta, Dk. Charles Msonde, wakati akitangaza matokeo ya mitihani ya Taifa ya kidato cha nne, darasa la nne na kidato cha pili jijini Dar es Salaam.

“Kati ya watahiniwa waliobainika kufanya udanganyifu, watahiniwa 77 ni wa darasa la nne, 63 ni wa kidato cha Pili na 75 ni wa Kidato cha nne,” amesema Dk. Msonde

Pia, Dk. Msonde amesema, baraza hilo limezuia kutoa matokeo ya watahiniwa 252 ambao walipata matatizo ya kiafya na kushindwa kufanya mtihani kwa masomo yote au idadi kubwa ya masomo.

“Watahiniwa husika wamepewa fursa ya kufanya mtihani kwa masomo ambayo hawakuyafanya kwa sababu ya ugonjwa mwaka 2021 kwa mujibu wa Kifungu cha 32(1) cha Kanuni za Mitihani.”

“Kati ya watahiniwa waliopewa fursa ya kurudia mitihani yao mwaka 2021, watahiniwa 17 ni wa kidato cha Pili na 235 ni wa kidato cha nne.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanawake GGML wawanoa wanafunzi Kalangalala Sec. kujitambua

Spread the loveKATIKA kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani, Umoja wa...

error: Content is protected !!