ALIYEKUWA Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi, Boniface Wambura amemaliza mkataba wake na amepewa kazi nyingine ndani ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kuwa Mkuu wa Idara ya Habari na Masoko ambapo atasaidiwa na Clinford Ndimbo na Aron Nyanda. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).
Katibu mkuu wa TFF, Wilfred Kidau amesema kuwa baada ya Wambura kumaliza mkataba wake kama muajiliwa ndani ya Bodi ya Ligi, Kamati ya Utendaji imeamua kumrudisha ndani ya Shirikisho kwa kuwa bado anauwezo mkubwa wa kuhudumu katika nafasi hiyo ya habari na masoko ili kuongeza ufanisi.
“Rais wa TFF, Walace Karia kwa kushirikiana na kamati tendaji wameamua kumteuwa Boniface Wambura kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Habari na Masoko akisaidiwa na Ndimbo kwenye upande wa habari na Aron Nyanda upande wa masoko ili kuongeza ufanisi katika shughuli za kila siku ndani ya shirikisho,” alisema Kidau.
Katibu aliendelea kusema kuwa nafasi ya mtendaji mkuu wa bodi ya ligi itatangazwa hivi karibuni kupitia vyombo vya habari.
Katika hatua nyingine Kamati ya utendaji imemteuwa Oscar Milambo kuwa Mkurugenzi wa Ufundi ya TFF akiziba nafasi iliyoachwa wazi na Ammy Ninje ambaye amerejea masomoni hivi karibuni.
Leave a comment