Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Waliotekeleza ghasia Cameroon wamtibua rais
Kimataifa

Waliotekeleza ghasia Cameroon wamtibua rais

Rais wa Cameroon, Paul Biya
Spread the love

RAIS wa Cameroon, Paul Biya amelaani ghasia zilizotekelezwa na wananchi na kusababisha mauaji ya watu nane wakati wa maandamano ya raia wa nchi hiyo, anaandika Catherine Kayombo.

Maandamano hayo yaliyofanywa  na wazungumzaji wa lugha ya kingereza nchini humo wanaotaka kujitenga na kupewa eneo lao, yaliingiliwa kati na polisi na kusababisha raia hao kupigwa risasi.

Ghasia hizi zimetokea wakati wa maadhimisho ya miaka hamsini na sita tangu kujumuishwa kwa jimbo la wazungumzaji wa kiingereza ndani ya Cameroon.

Aidha rais Biya amewataka wananchi kutotenganishwa na itifaki za lugha kati yao, na kudai kuwa mgogoro wa lugha unaweza sababisha vita ya wao kwa wao.

Wazungumzaji wa lugha ya kingereza nchini Cameroon kwa uchache wao wamekuwa wakiandamana takribani mwaka sasa wakidai kubaguliwa hasa katika mfumo wa elimu na sheria ukilinganisha na wale wanaozungumza lugha ya Kifaransa.

 

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!