Wednesday , 24 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya ‘Waliokuwa na dereva taxi Arusha, hawajaambukizwa COVID-19’
AfyaHabari Mchanganyiko

‘Waliokuwa na dereva taxi Arusha, hawajaambukizwa COVID-19’

Spread the love

DAKTARI Janeth Mghamba, Mkurugenzi Msaidizi wa Kitengo cha Ufutiliaji wa Magonjwa ya Mlipuko katika Wizara ya Afya amesema, watu 27 waliochukuliwa ili kupimwa kama wana maambukizi ya virusi vya corona jijini Arusha, wapo salama. Anaripoti Mwandishi Wetu, Arusha … (endelea).

Amesema, watu walioshukuliwa vipimo ni wale waliobainika kuwa na mawasiliana ama kukutana na dereva wa taksi ambaye alimbeba mgonjwa wa kwanza wa corona nchini.

Mbele ya waandishi wa habari leo tarehe 19 Machi 2020, akiambatana na Dk Faraja Msemwa ambaye ni Mtaalam wa Majanga wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Dk. Mghamba amesema sampuli za watu hao baada ya kupimwa walibaini kutoadhiriwa na virusi hivyo.

“Hawa walikuwa karibu na dereva na baada ya kuchukuliwa vipimo, wamebainika hawajaambukizwa,” amesema

Amesema, licha ya taarifa hiyo ya kutoathiriwa na virusi hivyo, wataendelea kufuatiliwa mpaka watakapopimwa kwa mara ya tatu kama ambavyo WHO iliagiza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

Habari Mchanganyiko

Watuhumiwa 12 wa kilo 726.2 za dawa za kulevya wafikishwa mahakamani

Spread the love  WATUHUMIWA watatu wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kibaha Mkoani...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!