Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Waliochoma Kituo cha Polisi  Bunju A wafungwa maisha
Habari Mchanganyiko

Waliochoma Kituo cha Polisi  Bunju A wafungwa maisha

Spread the love

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam leo tarehe 22 Februari 2019 imewafunga maisha jela watu wanane baada ya kukutwa na hatia katika kesi ya kuchoma moto Kituo cha Polisi cha Bunju A kilichopo jijini Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Hukumu hiyo iliyoacha simanzi imetolewa leo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba.

Akisoma hukumu hiyo, Hakimu Simba amesema kitendo cha watu hao kuchoma kituo hicho hakivumiliki na kushindwa kuwaonea huruma kutokana na kuhatarisha usalama wa nchi.

Washtakiwa hao walitekeleza tukio hilo tarehe 10 Julai mwaka 2010, ambapo walikuwa wanakabiliwa na mashtaka sita ikiwemo shtaka hilo la kuchoma moto kituo hicho.

Mbali na washtakiwa hao nane kufungwa maisha jela, Mahakama imewaacha huru watu 10  walioshtakiwa kwa kosa hilo. Awali wakati kesi hiyo inafunguliwa, kulikuwa na washtakiwa 35 ambapo 17 waliachwa huru na kubaki 18, ambapo leo hii kumi waliachwa huru pia baada ya kuonekana hawana hatia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Gardner Habash wa Clouds Fm afariki dunia

Spread the loveALIYEKUWA mtangazaji wa kipindi cha Jahazi kinachorushwa na kituo cha...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

error: Content is protected !!