Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Walimu walionyimwa stahiki zao wamchongea Mkurugenzi kwa Jafo
Elimu

Walimu walionyimwa stahiki zao wamchongea Mkurugenzi kwa Jafo

Suleiman Jafo, Waziri wa Tamisemi
Spread the love

WALIMU watano waliohamishwa kutoka kituo cha kazi cha shule ya sekondari Kisasa katika Jiji la Dodoma na kupangwa kwenye vituo vingine bila kulipwa stahiki zao za uhamisho, wamepeleka kilio chao kwa Waziri wa TAMISEMI, Suleiman Jafo. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Kutokana na hali hiyo walimu hao (wameomba majina yao yahifadhiwe) wamemuomba Waziri Jafo kuingilia kati jambo hilo kwani inaonekana kuna dalili za kutaka kufukuzwa kazi kwa mizengwe.

Hali hiyo imejidhiilisha baada ya walimu wa shule ya sekondari Kisasa Jijini Dodoma kuhamishwa na kupelekwa katika vituo vingine vya kazi bila kulipwa stahiki zao za uhamisho kama ilivyoelekezwa na Rais Magufuli.

Walimu hao walikuwa ni walimu wa shule hiyo na kuhamishwa kwa siku moja bila kulipwa stahiki zao za uhamisho, kama ilivyoagizwa na Rais Magufuli, alilolitoa Mei Mosi 2017 katika maadhimisho ya siku ya wafanyakazi wilaya Moshi Mkoani Kilimanjaro.

Maagizo hayo ya Rais ya kutaka watumishi kutohamishwa bila kulipwa stahiki zao iliwekewa mkazo na Waziri wa Jafo, wakati akijibu maswali ya wabunge bungeni wakati wa kipindi cha maswali na majibu alipokuwa akijibu maswali ni kwanini walimu na baadhi ya watumishi wamekuwa wakihamishwa bila kupewa stahiki zao za uhamisho.

Wakizungumza na MwanaHALISI Online walimu hao, walisema kuwa kitendo cha kuhamishwa bila kupewa fedha ni kwenda kinyume na utaratibu wa kazi.

Kwa Mujibu wa  walimu hao walipata walisema kuwa kwa pamoja walipata barua za uhamisho Julai 17 mwaka huu zenye maelezo kuwa uhamisho wao utagharamiwa na serikali jambo ambalo halijafanyika.

“Sisi walimu hatujakataa kuhama lakini hatujalipwa fedha zetu lakini hatuna fedha za kujikimu na vituo vipo mbali na hatuna hata fedha za kulipa kodi,” walisema walimu hao.

Wakiendelea kuelezea walimu hao walisema licha ya kutokulipwa stahiki zao za uhamisho walidai kuwa wamefikia hatua ya wakuu wa shule katika vituo vipya wamekuwa wakizuiliwa kusahini katika daftari ya Maudhurio.

Alipofafutwa Afisa Elimu Sekondari Jiji la Dodoma, Martin Nkwabi ili aweze kuelezea ni kwanini walimu hao wamehamishwa watano kwa wakati mmoja kutoka shule moja na kutokulipwa stahiki zao za uhamisho alijibu kuwa aulizwe Mkurugenzi wa Jiji ambaye ni Godwini Kunambi na kukata simu.

Alipotafutwa Mkurugenzi wa Jiji Godwini Kunambi, hakupokea siku na alipotumiwa ujumbe mfupi kwa simu ya kiganjani hakuweza kujibu.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Walimu (CWT) Mkoa wa Dodoma, Samson Mkotya, alisema kuwa hana imani kuwa kuna mtumishi ambaye anaweza kukaidi kutekeleza agizo lililotolewa na Rais Dk. John Magufuli na kuungwa mkono na Waziri wa TAMISEMI pamoja na kutolewa Maagizo na Waziri wa Utumishi na Utawala Bora.

“Napenda kusema kuwa walimu kuhamishwa kwa wakati mmoja siyo tatizo hiyo inatokana na mahitaji lakini kinachotakiwa ni kuwa na utaratibu ambao unatakiwa wa kuwahamisha walimu hao.

“Sipendi kuhamini kuwa ofisi ya Ofisa Elimu na ofisi ya Mkurugenzi ambao tumekuwa tukifanya nao kazi vizuri kwa kushirikiana wanawahamisha walimu hao bila kufuata utaratibu wa kisheria uliowekwa,” alieleza Mkotya.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanawake GGML wawanoa wanafunzi Kalangalala Sec. kujitambua

Spread the loveKATIKA kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani, Umoja wa...

error: Content is protected !!