Wednesday , 24 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Walimu Pemba wapigwa marufuku kwenda harusini
Habari Mchanganyiko

Walimu Pemba wapigwa marufuku kwenda harusini

Baadhi ya Walimu wa shule za sekondari na msingi mkoani Pemba
Spread the love

WALIMU wa Shule za msingi na sekondari katika mkoa wa Kaskazini Pemba visiwani Zanzibar wamepigwa marufuku kwenda katika sherehe hasa harusi wakati wa kazi. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Agizo hilo limetolewa leo na Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Omar Khamis Othman, kwa kusema kuwa serikali haitamvumulia mwalimu atakayetoroka shule kwenda harusini, na kwamba atakayebainika atachukuliwa hatua za kisheria.

RC Othman amesema kuwa, baadhi ya walimu wamekuwa na desturi ya kwenda harusini wakati wa muda wa kazi hasa siku za ijumaa, ambapo amekemea tabia hiyo kwa kuwa ni kinyume na sheria za utumishi wa umma.

Aidha, amewataka wakuu wa shule mkoani humo kutotoa ruhusa kwa walimu wenye tabia za kuondoka shule wakati wa kazi kwa ajili ya kwenda katika sherehe mbalimbali, na kuagiza walimu hao kama wanataka kwenda shughulini kusubiri muda wa kazi utakapoisha.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

error: Content is protected !!