Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Walimu 18,181 wameajiriwa 2015/20 – Serikali
ElimuHabari za Siasa

Walimu 18,181 wameajiriwa 2015/20 – Serikali

Prof. Joyce Ndalichako, Waziri wa Elimu
Spread the love

SERIKALI imeeleza, kuanzia mwaka 2015 mpaka 2020, sekta ya elimu imeajiri walimu 18,181. Shule ya Msingi 10,666, sekondari 7,218 na mafundi sanifu maabara 297. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Rashid alitaka kujua, lini na mkakati gani serikali imeweka ili kukabili upungufu wa walimu kwenye shule zake.

“Sekta ya elimu nchini inakabiliwa na uhaba wa walimu, Je, serikali imeweka mkakati gani wa kuziba pengo hilo la uhaba wa walimu,” amehoji Rashid Abdallah Shangazi, Mbunge wa Mlalo leo tarehe 14 Mei 2020.

Wizara imeeleza, “serikali itaendelea kuajiri walimu katika Sekta ya elimu kwa kadri ya upatikanaji wa rasilimali fedha,” imeeleza Wizara ya Elimu.

Pia Tunza Issa Malipo (Mbunge wa Viti Maalum – Chadema), amehoji idadi ya shule za sekondari zinazofundisha somo la TEHAMA.

Wizara hiyo imeeleza kwamba, Shule za Sekondari zinazofundisha somo la TEHAMA nchini ni 188. Shule 47 ni za serikali na 141 ni binafsi.

“Serikali inaendelea kuandaa mazingira wezeshi na kuimarisha eneo la rasilimali watu, kwa kuongeza walimu waliosomea Somo la TEHAMA.

“Imeendelea kuziwezesha Shule za Sekondari kuwa na vifaa vya

kisasa vya TEHAMA, kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ili kuziwezesha shule nyingi kufundisha somo hilo,” imeeleza wizara.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!