WAKULIMA Mkoani Morogoro wametakiwa kuchangamkia fursa ya kilimo cha pilipili kichaa kutokana na zao hilo kuwa na soko huku likiwa na sifa ya kutoshambuliwa na magonjwa. Anaripoti Christina Haule … (endelea).
Hayo yalisemwa Mwekezaji kutoka Kampuni inayojishughulisha na mazao ya kilimo biashara (Vergrab Organic Farming Limited), Josephat Ligondo wakati akizungumza na vikundi mbalimbali vya wakulima vilivyopo katika Manispaa ya Morogoro.
Ligondo alisema kuwa wakulima wanaweza kubadilika kifikra na kuanza kulima zao la pilipili kichaa ambalo lilikuwa likilimwa zamani na mababu zetu ambapo wakulima wakizingatia kilimo chakena kufuata ushauri wa wataalamu wa kilimo wataweza kuona manufaa yake.
Akitolea mfano Ligondo alisema, mkulima anaweza kuotesha miche ya pilipili 12,000 kwa hekari moja na kupata mavuno baada ya kukausha kg 150 kwa wiki moja ambayo mkulima anaweza kuuza shilingi 4,500 kwa kilo na kuweza kupata kiasi cha zaidi ya shilingi mil 2.7 kwa mwezi.
Aidha alisema kuwa wakulima wa zao hilo sasa wataweza kunufaika kufuatia kuwepo kwa kampuni hiyo ya kununua zao la pilipili ambalo lina masoko makuu katika nchi za Malawi , Zimbabwe,Kenya na Uganda .
‘’sisi tukiingia mikataba na wakulima tunanunua kila wiki tani 8 hadi 10 sasa ni vizuri wakulima wachangamkie fursa hiyo ya soko’’alisema Ligondo.
Hata hivyo Mwekezaji huyo alisema zao la pilipili kichaa lina manufaa mengi ikiwemo kutumika kwa ajili ya kutengeneza chakula cha watoto, dawa aina ya volin na mabomu ya machozi.
Kwa upande wake Mwakilishi kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa Evans manyanda alisema, kufuatia fursa hiyo ya soko la Pilipili iliyojitokeza Serikali ya mkoa itaangalia namna ya kujenga kituo maalumu cha kukaushia pilipili ili wakulima waweze kupelekea zao hilo kukausha na kuuza kwa urahisi baada ya kuingia mkataba maalumu na mwekezaji.
I AM ALSO INTERESTED TO GROW THIS CROP
Tatizo masoko hayo ni ya msimu Tu sio co masoko endelevu kama mikataba inavyosema
Njooni Lushoto
Habarini za leo, Mimi Ni mnunuzi Mkubwa wa pilipili kichaa na kwasasa natafuta Tani 100 za pilipili kichaa please mwenye nazo anitafute +255710507823
Mimi nahitaji pilipili kichaa tani 200 mawasiliano 0713828113
Mimi niko wilaya ya mufindi naweza kulima pilipili kichaa za kibiashara kwani nimijaribu zinastawi
Mimi ni mkulima nahitaji maelekezo ya kina, kuhusu zao hilo. 0786 950 181
Kuna aina fulani ya mbegu wanayohitaji, au ni kila iitwayo pilipili kichaa?
Pili, mbegu zinapatikana wapi?
Naomba mwenye ujuzi juu ya aina ya mbegu na soko pia anisaidie 0688409501
mnunuzi wa pilipili kichaa awasiliane nami 0714567798
Nahitaji mbegu
Ajuaye ipatikanapo mbegu na bei anijulishe no 0656697052
Mm ni mkulima nipo znz. Ss wapi branch yenu tutaipata pamoja na mbegu.
Mimi ni mkulima nishavuna na nishakausha Nina Kama kilo 400 store na bado navuna na ninauwakika wa kukausha Ila tatizo ni soko Kama Kuna mnunuzi naomba anitafute nipo pwani mwalusembe 0620475742