Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Wakulima wadogo wapigiwa debe kuhudhuria 88
Habari Mchanganyiko

Wakulima wadogo wapigiwa debe kuhudhuria 88

Spread the love

MKUU wa Idara ya mazao ya Utafiti wa kilimo Kanda ya Mashariki, Salvatory Kundi ameiomba Serikali kutafuta njia mbadala ya kuwawezesha wakulima wadogo kufika kwa wingi katika maonesho ya wakulima ya 88 kutokana na wakulima wakubwa kufika kwa wingi tofauti na kusudio la maonesho. Anaripoti Christina Haule … (endelea).

Kundi amesema maandalizi ya sherehe za wakulima Nanenane Kanda ya Mashariki 2018 yatakayofanyika kwenye viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere vya Maonesho ya wakulima 88 vilivyopo Tungi nje kidogo ya mji wa Morogoro, yamekamilika.

Amesema kuwa kwa muda mrefu sasa wamekuwa wakiona wakulima wakubwa na wakati kwa wingi wakifika kupata elimu katika mabanda yao tofauti na wakulima wadogo ambao ndio wengi na ndio lengo hasa la dhana ya kilimo kumyanyua mkulima mdogo.

Kundi amesema kuwa hali ya wakulima wadogo kutoonekana wengi kwenye maonesho hayo na kujipatia ujuzi wa kilimo bora inatokana na kuwepo kwa viingilio kwenye maonesho getini na gharama za usafiri kutoka mahali walipo hadi kwenye maonesho hayo.

“Utakuta mkulima anatoka kijijini na ili aweze kujifunza na kupata uelewa itabidi atumie muda kuwepo uwanjani sasa atalala wapi, atafikaje uwanjani kulingana na changamoto za usafiri na kiingilio,” amehoji Kundi.

Akizungumza kwenye upandaji vipando hivyo Mkurugenzi wa utafiti na maendeleo Kanda ya Mashariki kutoka Wizara ya Kilimo, Dk. Geoffrey Mkamilo amewataka wakulima nchini kuhakikisha wanapofika kwenye maonesho hayo wanazitumia vyema taasisi za utafiti wa kilimo zinazowekeza katika kujifunza teknolojia mbalimbali za uzalishaji wa mazao ya kilimo zinazotolewa ili waweze kuzalisha kwa tija na kuachana na kilimo cha kizamani.

Dk. Mkamilo amesema kuwa Wizara ya Kilimo ina idara ya utafiti na maendeleo ambapo inafanya shughuli za utafiti wa mazao mbalimbali ili kumwezesha mkulima kuweza kuzalisha kwa tija ambapo katika Kanda ya Mashariki yapo mazao yanayoratibiwa kitaifa na kikanda.

Ameyataja mazao ya kitaifa yanayoratibiwa na Ilonga kuwa ni pamoja na zao la mahindi katika ukanda wa chini na wakati, mazao ya jamii ya mikunde huku ya kitaifa yakiwa ni mtama ,uwele ,ulezi ,mihogo na jamii ya viazi.

Amesema kuwa katika kazi za utafiti wanaainisha teknolijia mbalimbali kwa ajili ya wakulima na wadau katika kujua teknolojia ya mbegu bora za mazao husika na pia kuwafundisha teknolojia ya usindikaji wa mazao mbalimbali ili kuweza kuwa na bidhaa mbalimbali kupitia mazao wanayozalisha.

“Teknoloji hizi zina faida kubwa kwa wakulima endapo watazizingatia kwani mbegu zinauwezo wa kuzaa kwa wingi na pia zina sifa ya kuzaa kwa muda mfupi na kuvumilia ukame na ili mkulima aweze kuona ubora wa elimu hiyo ni lazima mazao hayo yaweze kupandwa maelkezosahihi ya watafiti kulingana na muda wa upandaji,” amesema Dk. Mkamilo

Naye Mratibu wa usambazaji wa teknolojia za kilimo Kanda ya Mashariki, Margaret Mchomvu amesema kuwa wanaotesha mazao ya aina mbalimbali ili inapofika kipindi cha maonyesho ya Nanenane mazao hayo yaweze kuwa tayari yamekomaa ili kuwawezesha wakulima kujifunza kwa uhalisia sambamba na kuona namna mazao yanavyosindikwa katika mabanda yao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Puma Energy Tz: Watanzania tudumishe amani kuvutia uwekezaji

Spread the loveKAMPUNI ya Mafuta ya Puma Tanzania imewakutanisha wadau mbalimbali katika...

Habari Mchanganyiko

DAWASA waanza utekelezaji agizo la Samia

Spread the loveMamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam...

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

error: Content is protected !!