WAKULIMA wa Mkoa wa Dodoma wametakiwa kulima mazao ambayo yanaendana na hali ya hewa ili kuweza kupata mazao mengi. Anaripoti Dany Tibason, Dodoma … (endelea).
Wito huo umetolewa na Afisa kilimo Mkoa wa Dodoma, Brnard Abraham alipokuwa akizungumaza na waandishi juu ya uhamasishaji wa kilimo chenye tija kwa wakulima wa Mkoa wa Dodoma.
Mbali na kuwataka wakulima kulima mazao ambayo yanaendana na hali hewa pia amewataka wataalamu wote wa kilimo kuwa karibu na wakulima kwa maana ya kuhamishia ofisini mashambani kwa lengo la kuwasaidia wakulima ndani ya Mkoa huu.
Abraham alisema kuwa yapo malalamiko kuwa wataalamu wa kilimo ni wachache katika maeneo ya mashamba jambo ambalo alisema kuwa kwa Tanzania hakuna sekta yoyote ambayo imejitoshereza lakini watumishi au wataalamu wamekuwa karibu na wadau wao.
“Kipindi hiki ni kipindi cha maadalizi ya mashamba hivyo nawashauri wakulima kulima kilimo ambacho kinaendana na mazingira husika kutokana na hali ya hewa, wapo wakulima ambao wanalazimisha kulima mazao ambayo hayaendani na hali ya hewa husika.
“Ni lazima kulima kilimo chenye tija na kinachoweza kumuinua mkulima kimaisha na taifa kwa ujumla wake lakini kama wataendelea kulima kilimo ambacho ni cha mazoea ni wazi kuwa wataendelea kulima kilimo cha kujikimu badala ya kuwa na kilimo chenye tija.
“Hata hivyo nawaagiza wataalamu wa kilimo kuwa karibu na wakulima kwa maana ya kuwaelekeza ni jinsi gani ya kuwashauri wakulima ili walime kilimo cha kisasa na chenye tija badala ya kulima maeneo makubwa lakini hayana tija na mazao wanayovuna ni kiduchu,” alisema Abraham.
Katika hatua nyingine Abraham alisema pia wakulima wana wajibu wa kuwa karibu na wataalamu wa kilimo pale wanapokuwa wakihitaji ushauri au maelekezo au pale wanapoona kuwepo kwa dalili wazizozielewa ili waweze kupatiwa ushauri.
Leave a comment