Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Wakimbizi wa Burundi waanza kurejea kwao
Kimataifa

Wakimbizi wa Burundi waanza kurejea kwao

Spread the love

AWAMU ya kwanza ya wakimbizi wa kutoka Burundi wanaorejea kwa hiari yao kutoka Tanzania wanatarajiwa kuwasili nchini mwao hii leo, anaandika Jovina Patrick.

Hatua hiyo imefikiwa baada ya makubaliano wiki iliyopita kati ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR), Tanzania na Burundi.

Abel Mbilinyi, Mwakilishi Mkazi wa UNHCR nchini Burundi amethibitisha kurejea kwa wakimbizi 300 nchini humo.

Wakimbizi hao wanafuikia katika vinne vilivyo katika maeneo ya mashariki na kusini mwa Burundi pamoja na mji mkuu Bujumbura.

Inakadiriwa kwamba hadi kufikiab mwisho wa mwaka huu, wakimbizi 12,000 wa Burundi wanaoishi Tanzania watakuwa wamerejea kwao.

Kuna wakimbizi takribani 250,000 wa Burundi katika kambi mbali mbali hapa nchini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!