Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Maisha Elimu ‘Wahitimu Kidato cha IV wachangamkie fursa hii’
Elimu

‘Wahitimu Kidato cha IV wachangamkie fursa hii’

Wanafunzi
Spread the love

WANAFUNZI waliomaliza Kidao cha IV mwaka 2018 na matokeo yao kutangazwa, sasa wanaweza kutumia mfumo maalumu kubadili chaguo za masomo na tahasusi kulingana na ufaulu wa mitihani yao, kabla ya kupangiwa shule ama vyuo. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Serikali imetoa fursa hiyo ili kuongeza wingi kwa mwanafunzi kusoma fani au tahasusi itakayomuandaa kuwa na utaalamu fulani katika maisha yake.

Seleman Jafo, Waziri wa Nchi,  Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na waandishi wa habari kusudiuo la serikali kutoa fursa hiyo ya kufanya mabadiliko ya machaguo kwa utaratibu wa kujaza fomu inayoitwa ‘F4 Selform.’

Jafo amesema, fursa hiyo itawawezesha wanafunzi kurekebisha machaguo yao kulingana na ufahulu waliopata kwenye matokeo ya kidato yao yaliyopita hasa baada ya kujua masomo waliyofaulu vizuri.

“Hii ni kutokana na ukweli kwamba, baadhi ya wanafunzi hawakujaza kwa uhakika tahasusi au kozi zao kutokana na kutokuwa na uhakika wa ufaulu katika masomo yao.

“Serikali kupitia TAMISEMI, imekamilisha zoezi la awali la kuingiza taarifa zilizo kwenye Selform za wanafunzi kwenye kanzi data ya TAMISEMI kama zilivyojazwa wakiwa shuleni kabla ya kuhitimu,” amesema Jafo.

Amesema, kwa sasa wanafunzi wataweza kufanya mabadiliko hayo kwa njia ya mtandao kadri watakavyonuia au kushauriwa. Na baada ya wanafunzi kufanya marekebisho hayo, kanzi data hiyo ndiyo itakayotumika kuwachagua na kuwapangia kidato cha tano na kozi za vyuo.

“Ili mwanafunzi aweze kuingia kwenye mfumo huu, itabidi kutumia namba ya mtihani wa kuhitimu Kidato cha Nne, mwaka 2018, jina lake la mwisho, mwaka wa kuzaliwa na alama ya ufaulu aliyopata kwenye somo atakaloulizwa na mfumo au swali lolote atakaloulizwa.

“Ni matumaini yangu, watahitimu watatumia kwa ukamilifu fursa waliyopewa ya kubadilisha tahasusi na kozi kulingana na ufaulu walioupata ili waweze kusoma kozi au tahasusi ambazo wamefaulu vizuri,” alisema Jafo.

Amesema, zoezi hilo la kubadili tahasusi litafanyika kuanzia tarehe 1-15 Aprili 2019. Kutokana na muda huo uliopangwa kwa yeyote ambaye hatabadili taarifa zake TAMISEMI, itaamini kwamba ameridhika na machaguo yake ya tahasusi aliyofanya awali alipokuwa shuleni.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanawake GGML wawanoa wanafunzi Kalangalala Sec. kujitambua

Spread the loveKATIKA kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani, Umoja wa...

error: Content is protected !!