Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wahariri, Waandishi wamsusia Makonda
Habari MchanganyikoTangulizi

Wahariri, Waandishi wamsusia Makonda

Paul Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam
Spread the love

JUKWAA la Wahariri Tanzania (TEF) na Klabu ya Waandishi wa Habari wa Mkoa wa Dar es Salaam (DCPC), wameazimia kumnyima Paul Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, ushirikiano wa kibahari kwa kutoandika au kutangaza habari zote zinazomhusu, anaandika Pendo Omary.

TEF na DCPC wamechukua hatua hiyo, baada ya Makonda kuvamia kituo cha habari cha Clouds Media, kilichopo Mikocheni, kiasi cha saa 5 usiku, Ijumaa ya wiki iliyopita, akifuatana na polisi wenye silaha na kutaka kulazimisha kurushwa kipindi cha SHILAWADU kwa namna atakavyo.

Taarifa ya asasi hizo za wanahabari imetolewa leo jijini Dar es Salaam na Theophil Makunga, Mwenyekiti wa TEF, na Jane Mihanji, Mwenyekiti wa DCPC, na kuungwa mkono na Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC).

“Kwa pamoja tumeazimia kutoandika habari zote zinazomhusisha Makonda katika vyombo vyetu vya habari. Kwa mantiki hiyo tunamtangaza Paul Makonda kuwa ni adui wa uhuru wa habari na yeyote yule ambaye anashirikiana au atashirikiana naye katika kukandamiza uhuru wa vyombo vya habari,” inasomeka sehemu ya taarifa hiyo.

Taarifa inasema utekelezaji wa azimio hilo unaanza mara moja kwa vyombo vyote vya habari nchini na utaendelea hadi pale itakapotangazwa au kuagizwa vinginevyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!