Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wagonjwa wa corona Tanzania waongezeka
Habari MchanganyikoTangulizi

Wagonjwa wa corona Tanzania waongezeka

Spread the love

IDADI ya wagonjwa wa Homa Kali ya Mapafu inayosababishwa na  Virusi vya Corona (COVID-19), nchini Tanzania wamefika 19. Inaripoti Regina Mkonde…(endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo tarehe 30 Machi 2020 na Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.

Waziri Ummy amesema, wagonjwa watano wapya, watatu wanatoka jijini Dar es Salaam na wawili wanatoka visiwani Zanzibar.

“Ninapenda kutoa taarifa kwamba leo tumethibitisha kuwepo kwa wagonjwa wapya watano wa COVID-19, baada ya kufanyiwa vipimo katika maabara yetu Kuu ya Taifa, Hivyo sasa jumla ya wagonjwa wa COVID-19 nchini ni 19,” amesema Waziri Ummy.

Akitoa ufafanuzi wa wagonjwa hao, Waziri Ummy amesema mmoja mwanaume mwenye umri wa miaka 49 alipata maradhi hayo baada ya kukutana na raia wa kigeni aliyetoka nchi zilizoathirika zaidi. Wakati mwingine ni mwanamke mwenye umri wa miaka 21.

“Mwingine ni mwanaume mwenye umri a miaka 49, Mtanzania ambae pia ni miongoni mwa watu waliokuwa wakifuatiliwa,” amesema Waziri Ummy.

Waziri Ummy amesema kazi ya kufuatilia watu wote wa kjaribu waliokutana na wagonjwa hao inaendelea, na kuwataka wananchi kuchukua tahadhari zaidi juu ya mamabukizi ya ugonjwa huo.
Wakati Tanzania ikitangaza kwamba ina wagonjwa 19, Rwanda mpaka sasa wana jumla ya wagonjwa 70.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!