Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Maisha Afya Wagonjwa mil 1.3 wa corona wapona duniani
Afya

Wagonjwa mil 1.3 wa corona wapona duniani

Spread the love

WAGONJWA 1,394,965 kati ya 4,030,053 waliokuwa wameambukizwa virusi vya corona (COVID-19) wamepona ugonjwa huo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Ugonjwa huo ulioanzia mji wa Wahun nchini China mwishoni mwa mwaka 2019, umesambaa mataifa mbalimbali dunia na hadi leo Jumamosi tarehe 9 Mei 2020 saa 7.50 mchana umesababisha vifo vya watu 276,498.

Kwa mjibu wa mtandao wa Worldmeter inaonyesha hadi muda huo wagonjwa ni 2,358,590 kati yao 2,310,087 sawa na asilimia 98 wanaendelea vizuri huku 48,503 sawa na asilimia 2 wako katika hali mbaya.

Mtandao huo unaonyesha Marekani ndiyo taifa linaongoza kwa kuwa na maambukizi mengi yanayofikia 1,322,164 huku vifo vikiwa 78,616 na wagonjwa 223,749 wakipona.

Hispania inashika nafasi ya pili dunia ikiwa na wagonjwa 260,117. Kati yao wagonjwa 26,299 wamefariki dunia 168,408 wakipona.

Italia ina wagonjwa 217,185 ambapo vifo ni 30,201 na wagonjwa 99,023 wamepona. Uingereza ina wagonjwa 211,364 huku vifo vikiwa 31,241.

China ambako ugonjwa ulianzia, maambukizi ni 82,887 na vifo vikiwa 4,633 huku waliopona 78,046.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

Marekani kuipa Tanzania bilioni 980 kudhibiti VVU, UKIMWI

Spread the loveSERIKALI ya Tanzania inatarajiwa kupewa msaada wa fedha kiasi cha...

AfyaHabari Mchanganyiko

Wanavijiji wajenga zahanati kukwepa umbali mrefu kupata huduma

Spread the loveWANAVIJIJI wa Kata ya  Musanja Jimbo la Musoma Vijijini, mkoani...

AfyaTangulizi

Wanasayansi wagundua teknolojia ya kunyofoa VVU kutoka kwenye seli

Spread the loveTIMU ya wanasayansi kutoka Chuo Kikuu cha Amsterdam cha nchini...

Afya

Wananchi 530,000 kufaidika na ujenzi wa hospitali ya bil. 1.8

Spread the love  SERIKALI imetoa Sh 1.8 bilioni kwa ajili ya ujenzi...

error: Content is protected !!