Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Wagombea CCM watishiwa nyau Dodoma
Habari za Siasa

Wagombea CCM watishiwa nyau Dodoma

Spread the love

MCHAKATO wa kumpata Naibu Meya wa Manispaa ya Dodoma ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), umeanza huku wagombea waliojitokeza katika kinyang’anyiro hicho wakionywa kutokujihusisha na vitendo vya rushwa, anaandika Mwandishi Wetu.

Akizungumzia mchakato huo, Katibu wa CCM wilaya ya Dodoma, Pili Mbanga, amesema mchakato huo umeanza baada ya Mkurugenzi wa Manispaa hiyo kuwaandikia barua ya kuwasilisha jina la mgombea.

“Mchakato huu ndani ya chama utamalizika ndani ya wiki hii kwa kuwa maelekezo ya Mkurugenzi jina linatakiwa kuwasilishwa Agosti 9, mwaka huu,” amesema Katibu huyo.

Alibainisha hadi sasa wamejitokeza madiwani sita katika kinyang’anyiro hicho akiwemo Naibu Meya wa sasa, Jumanne Ngede anayetetea nafasi hiyo.

Aliwataja wengine ni Msinta Mayaoyao, Ally Mohamed, Abel Shauri, Jakobu Lemanya na Neema Mwaluko.

Aliwataka kutotumia rushwa katika uchaguzi huo kwa kuwa kiongozi mzuri anapatikana bila rushwa.
“Hawatakiwi kutoa au kupokea rushwa na ikibainika ameshinda kwa kutumia rushwa CCM itamuengua,” amesema Mbanga

Kadhalika, Mbanga amesema mchakato wa chaguzi mbalimbali ndani ya chama na jumuiya zake unaendelea na unatarajiwa kukamilika Agosti 5, mwaka huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Mwakyembe : Zanzibar waliongoza kutaka Serikali 2 za muungano

Spread the love  MWANASIASA mkongwe nchini, Dk. Harrison Mwakyembe, amesema mjadala wa...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

error: Content is protected !!