Tuesday , 19 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Waganga wamtuhumu Katibu kutumia madaraka vibaya
Habari Mchanganyiko

Waganga wamtuhumu Katibu kutumia madaraka vibaya

Spread the love

BAADA ya kufanyika kwa mkutano mkuu wa Umoja Chama Waganga wa Tiba Asilia, Wakunga (UWAWATA “T”) kukutana na kufanya mageuzi kwa kuondoa uongozi uliopita kwa kumtuhumu Katibu Mkuu wa Chama hicho Dk. Daud Nyaki kwa kufanya ubadhilifu na kuiganganya serikali naye ameibuka na kuwatukana wanachama hao kuwa ni wafu wa akili. Anaripoti Dany Tibason … (endelea).

Hali hiyo ya Katibu Mkuu Dk. Nyaki kuwatukana wenzake ni kutokana na mkutano mkuu wa kitaifa wa chama hicho ulioketi jana ya kata Kibaigwa kwa lengo la kujadili mwenendo wa viongozi hao waliokaa miaka kumi bila kufanya maendeleo yoyote na badala yake wamekisababishia chama hicho hasara.

Katika mkutano huo uliowakutanisa viongozi wa chama hicho kutoka mikoa mbalimbali wamesema kuwa uongozi ambao ulikuwa ukiendeshwa na katibu Mkuu Dk. Nyaki, umeshindwa kufanya kazi kwa zaidi ya miaka kumi na badala amekuwa akitumia madaraka yake vibaya kwa kuwalazimisha viongozi wa chama hicho kuchanga fedha kwa ajili ya matumizi yake binafsi.

Mmoja wa Makatibu wa chama hicho Kutoka Shinyanga aliyejitambulisha kwa jina la Shidula Mapalala, amesema Dk. Nyaki amechangisha kiasi cha zaidi ya Sh. 18 milioni kwa lengo la kuwanunulia walemavu wa ngozi (Albino) magari lakini hakuweza kufanya hivyo.

“Huyu aliyekuwa katibu mkuu wa chama hiki Dk. Nyaki alikuja Shinyanga na kulazimisha kila mganga kuchangia fedha kwa ajili ya kuwanunulia wengetu maalubino magari na hiyo ilitokana na kuwepo kwa mahusiano mazuri kati ya waganga wa tiba asilia na maalbino.

“Awali waganga wa tiba asilia tulishambuliwa sana na serikali pamoja na watu binafsi kuwa tnahusika katika mauaji ya maalbino na vikongwe kwa kuona hivyo tukajenga mahusiano mazuri ya waganga wa tiba asilia na watu wa jamii hiyo,kwa nafasi hiyo Dk.Nyaki alitumia nafasi hiyo kujikusanyia pesa nyingi kutoka kwa waganga wa tiba asilia kwa madai kuwa anataka kuwanunulia gari jambo ambalo halikufanyika.

“Zaidi ya Sh. 18 milioni zilichangwa lakini hakuna jambo lolote lililofanyika hakuna pesa iliyotumiwa, amezitumia kwa faida yake mwenyewe na unapojaribu kuhoji anakuja juu na kutishia kukufukuza kazi jambo hili sasa linakera sana na serikali inatakiwa kutambua kuwa mtu huyu anawavuruga waganga wa tiba asilia na kuonekana hawafahi,” amesema Mapalala.

Naye Mwenyekiti wa kanda ya ziwa na mwenyekiti wa uongozi wa mpito wa chama hicho, Bujukano Mahungu John lengo la kikao kilichofanyika ni kujadili mwenendo wa viongozi wa chama hicho waliovuka muda wao.

Bujukano amesema kuwa viongozi hao wakiongozwa na katibu mkuu wa chama hicho Dk. Nyaki kwa sasa hawana sifa ya kuendelea kuwa viongozi kwani wameisha vunja katiba ya chama hicho kwani uongozi ni wa miaka mitano na baada ya hapo kunafanyika uchaguzi.

Jambo lingine amesema kuwa kiongozi huyo amekuwa akilazimisha viongozi kuchangisha fedha kwa ajili ya ununuzi wa vifaa mbalimbali vya watu wenye ulemavu wa ngozi lakini amekuwa akikusanya fedha hizo bila kufanya jambo lolote na kueleza kuwa mbaya zaidi ni kuwatishia viongozi pale wanapojaribu kuhoji mabo ya msingi.

Aidha amesema kuwa Dk. Nyaki kwa uongozi wake wote a miaka 10 hajawahi kutoa taarifa ya mapato na matumizi na kuongeza kuwa kutokana na hali hiyo mkutano mkuu huo uliohsisha mikoa 11 ya Tanzania bara wamefanya mageuzi na kuweka viongozi wapya pamoja na kuunda kamati ya kufuatilia mali za chama na kuchukua hatua kali za kisheria.

Viongozi wa mpito waliochaguliwa ni Bujukano Mahungo John ambaye ni mwenyekiti, Licas Mlipu- Katibu, Maiko Salali- Mratibu, Mwanahamisi Kapera –Mratibu ukaguzi, Shida Twahibu –Katibu Mwenezi, Mrumba Abdul, Mkurugenzi Mashitaka, Mwajabu Mgaza-Mhasibu na Alex Raymond-Mjumbe.

Kwa pamoja viongozi hao paamoja wajumbe wametangaza rasmi kwa kutowatambua viongozi waliopita na kuitaka serikali kutowakumbatia viongozi hao kwani wamekuwa wakipaka matope chama.

Kwa upande wake katibu wasiyemtambua Dk. Nyaki alipoulizwa juu ya kukaa kwa mkutano mkuu na kumkataa yeye pamoja na uongozi wake amesema watu hao wameisha kufa na akili zao.

Amesema kinachofanyika ni unafiki na chuki na wala hajawahi kuchukua fedha za chama na wala kuchangisha fedha kwa mtu yoyote.

“Kwanza kabisa futa kauli yako mimi bado ni katibu mkuu hao waliokaa ni wahuni tu na wanafiki mimi sijawahi kuchangisha fedha wanaozungumza hivyo ni wale ambao walishafukuzwa kazi kutokana na utovu wa nidhamu ndani ya chama.

“Kuhusu hizo pesa mimi likaa Shinyanga zaidi ya miezi 4 na nlikuwa nadaiwa zaidi ya sh.Milioni 1.8 na nilienda nkalipa sikucangisha fedha, uongozi wa Shinyanga ulishindwa, lakini kama suala ni kutoa zawadi kwa Albino mimi ndiye niliyekuwa napendekeza kutoa zawadi hivyo silazimishwi kutoa misaada kwa Maalbino ila nilitoa sehemu mbalimbali,” amesema Dk.Nyaki.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Diwani, wananchi wengine 463 wahama Ngorongoro

Spread the loveMakamu mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Ngorongoro ambaye pia...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Shule zafungwa kutokana na ongezeko la joto

Spread the loveSUDAN Kusini imeamuru kufungwa kwa shule zote kuanzia leo Jumatatu,...

Habari Mchanganyiko

Bunge laja na Marathon kuchangia ujenzi wa sekondari

Spread the loveBUNGE la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linatarajia kukusanya fedha...

error: Content is protected !!