Wednesday , 24 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Waganga wa kienyeji mbaroni Mwanza
Habari Mchanganyiko

Waganga wa kienyeji mbaroni Mwanza

Spread the love

JESHI la Polisi mkoani Mwanza linawashikilia watu watatu kwa kosa la kufanya shughuli za uganga wa kienyeji bila kibali. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Akizungumza na wanahabari leo tarehe 8 Agosti 2018, Kamanda wa Polisi Mwanza, DCP Ahmed Msangi watuhumiwa hao, John Luzaria, Masanja Majige na Mariamu Ramadhani, wote wakazi wa Kijiji cha Mahando walikamatwa jana.

DCP Msangi amesema watuhumiwa hao pia walipatikana na vifaa vya kupigia ramli chonganishi .

“Watuhumiwa hao wanashikiliwa na jeshi la polisi kwa kosa la kupatikana na vifaa vya kupigia ramli chonganishi na kufanya shughuli za uganga wa kienyeji bila kibali, kitendo ambacho ni kosa kisheria,” amesema DCP Msangi.

DCP Msangi amesema Polisi wapo katika upelelezi na mahojiano na watuhumiwa wote watatu, na kwamba pindi uchunguzi ukikamilika watuhumiwa wote watafikishwa mahakamni.

“Aidha upelelezi na msako wa kuwatafuta watu wengine wanaojihusisha kwa namna moja au nyingine kufanya shughuli za uganga wa kienyeji bila kibali pamoja na upigaji wa ramli chonganishi katika maeneo hayo bado unaendelea,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

Habari Mchanganyiko

Watuhumiwa 12 wa kilo 726.2 za dawa za kulevya wafikishwa mahakamani

Spread the love  WATUHUMIWA watatu wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kibaha Mkoani...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari Mchanganyiko

GGML yasisitiza kuendelea kuimarisha afya za wafanyakazi

Spread the loveKAMPUNI ya Geita Gold Mining Limited kwa kushirikiana na kampuni...

error: Content is protected !!