JESHI la Polisi mkoani Mwanza linawashikilia watu watatu kwa kosa la kufanya shughuli za uganga wa kienyeji bila kibali. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).
Akizungumza na wanahabari leo tarehe 8 Agosti 2018, Kamanda wa Polisi Mwanza, DCP Ahmed Msangi watuhumiwa hao, John Luzaria, Masanja Majige na Mariamu Ramadhani, wote wakazi wa Kijiji cha Mahando walikamatwa jana.
DCP Msangi amesema watuhumiwa hao pia walipatikana na vifaa vya kupigia ramli chonganishi .
“Watuhumiwa hao wanashikiliwa na jeshi la polisi kwa kosa la kupatikana na vifaa vya kupigia ramli chonganishi na kufanya shughuli za uganga wa kienyeji bila kibali, kitendo ambacho ni kosa kisheria,” amesema DCP Msangi.
DCP Msangi amesema Polisi wapo katika upelelezi na mahojiano na watuhumiwa wote watatu, na kwamba pindi uchunguzi ukikamilika watuhumiwa wote watafikishwa mahakamni.
“Aidha upelelezi na msako wa kuwatafuta watu wengine wanaojihusisha kwa namna moja au nyingine kufanya shughuli za uganga wa kienyeji bila kibali pamoja na upigaji wa ramli chonganishi katika maeneo hayo bado unaendelea,” amesema.
Leave a comment