Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Wafungwa wateka gereza, watoa masharti mazito
KimataifaTangulizi

Wafungwa wateka gereza, watoa masharti mazito

Pingu
Spread the love

KATIKA hali isiyo ya kawaida, wafungwa wanaoshikiliwa kwenye gereza la Juba nchini Sudan Kusini wanadaiwa kuliteka gereza hilo huku wakiwa na silaha ikiwemo bunduki na visu, wakishinikiza kuachiliwa huru kwa wafungwa wa kisiasa. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Kwa mujibu wa mtandao wa BBC Swahili, umeripoti kwamba wafungwa hao ambao idadi yao rasmi haijajulikana, walimzidi nguvu mlinzi wa lango la kuingilia la gereza walilokuwamo kisha kuvunja milango kwa risasi, na kufanikiwa kuchukua bunduki na visu kutoka ndani ya ghala la kuhifadhia silaha.

Wafungwa hao wanadaiwa kuchukua hatua hiyo ikiwa ni sehemu ya shinikizo kwa Rais wa Sudan Kusini, Salva Kiir la kumtaka kutekeleza ahadi yake ya kuwaacha huru wafungwa wa kisiasa. Na kwamba mamlaka nchini humo inaendelea na mazungumzo dhidi ya wafungwa hao waliojihami kwa silaha.

Jeshi la Polisi nchini humo limekanusha madai hiyo, likieleza kuwa wafungwa takribani 60 kati ya 400 walioko kwenye gereza hilo, ndiyo walioanzisha vurugu hizo na mgomo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Chadema: Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

KimataifaTangulizi

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the love  TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

error: Content is protected !!