Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Wafanyakazi Azam wafariki ajalini
Habari MchanganyikoTangulizi

Wafanyakazi Azam wafariki ajalini

Spread the love

WAFANYAKAZI watano wa Azam Televishen kati ya saba leo tarehe 8 Julai 2019, wamepoteza maisha kwenye ajali iliyotokea katika eneo la Malendi, Wilaya ya Iramba mkoani Singida. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Kwenye ajali hiyo, watu watatu wamejeruhiwa. Akizungumza kuhusu tukio hilo, Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Singida, Sweetbeart Njewike amesema, ajali hiyo imetokea saa 2 asubuhi baada ya gari lao aina ya Coaster kugongana na lori.

“Ni kweli ajali imetokea majira ya saa 2 asubuhi, Coaster iliyokuwa inatoka Dar es Salaam kuelekea Mwanza iligongana na Roli lililokuwa linatoka Igunga kwenda Dar es Salaam. Watu saba wamefariki baadhi yao ni wafanyakazi wa Azam TV,” amesema Kamanda Njewike.

Kamanda Njewike amesema, Jeshi la Polisi linaendelea kufuatilia tukio hilo, ikiwemo chanzo cha ajali na majina ya waliofariki, na kwamba baada ya uchunguzi kukamilika watatoa taarifa.

Merichad Magongo, Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Igunga amethibitisha kwamba, wamepokea majeruhi watatu wa ajali hiyo.

Wanyakazi wanaotajwa kufariki kwenye ajali hiyo ni Said Haji, Charles Mwandwi, Salim Mhando, Frolence Ndibalema, Silvanus Kasongo. Majeruhi ni Mohamed Mwishehe, Mohammed Mainde na Artus Massawe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

error: Content is protected !!