Thursday , 18 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wadhamini wa Lissu ngoma mbichi
Habari Mchanganyiko

Wadhamini wa Lissu ngoma mbichi

Robert Katula, mdhamini wa Tundu Lissu akitoka mahakamani
Spread the love

WADHAMINI wa Tundu Lissu, aliyekuwa Mbunge wa Singida Mashariki, wamegomewa maombi yao kwamba ‘Lissu akamatwe’ waliyoyafikisha katika Mahakama Kuu ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam. Anaandika Faki Sosi, Dar es Salaam…(endelea).

Upande wa mashtaka umetaka ombi la wadhamini wa Lissu lifutwe ambapo jana tarehe 14 Julai 2020,  Wakili wa Serikali Mkuu Simon  Wankyo,  mbele ya Hakimu Mkazi   Mkuu Thomas Simba aliitaka mahakama hiyo kutotoa hati ya kukamatwa kwa Lissu ambaye kwa miaka mitatu, amekuwa nje ya nchi kwa ajili matibabu ya majeraha ya risasi.

Lissu alishambuliwa kwa risasi 16, alipokuwa anawasili nyumbani kwake Area ‘D’ jijini Dodoma akitoka bungeni tarehe 7 Septemba 2017.

Ombi hilo lilifunguliwa na Robert Katula na Ibrahim Ahmed, waliomdhamini kwenye kesi namba 208 ya 2016 inayohusu tuhuma za uchochezi dhidi yake na wahariri wa gazeti la Mawio pia mchapishaji wake.

Kesi hiyo inamuhusu Mhariri wa Mawio Simon Mkina, mwandishi mwandamizi Jabir Idrissa na mchapishaji wa Kampuni yaFlint, Ismail Mehboob.

Wankyo alieleza mahakama kwamba, dhamira ya kupinga ombi la wadhamini wa Lissu na kuwa, upande huo umepanga kuwalisilisha kwa maandishi na kuomba muda wa kuandaa hoja zao.

Wankyo amedai, mahakama hiyo tayari imeamua kuhusu ombi la kukamatwa kwa Lissu na kwamba  ililiondoa.

Hakimu Simba amesema, mawasilisho ya hoja za serikali yafanywe ifikapo tarehe 28 Julai 2020 na waombaji wajibu tarehe 11 Agosti na kutakuwa na haja ya kujibu upande ufanye hivyo tarehe 18 Agosti 2020. Usikilizaji utafanyika tarehe 19 Agosti mwaka huu.

Kwenye kesi ya msingi, watuhumiwa wanashtakiwa kwa mashtakamatatu ya uchochezi kupitia gazeti la Mawio kwa kuchapisha habari yenye kichwa ‘Machafuko yaja Z’bar.’ Watuhumiwa wote wapo nje kwa dhamana ,

Kukosekana kwa Lissu kesi hiyo inapotajwa kumechangia mahakaa kuwabana wadhamini wamfikishe mahakamani mtuhumiwa kwa kuwa ndio jukumu lao kisheria.

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

Habari Mchanganyiko

Serikali yatoa ajira watumishi 46,000, yatangaza utaratibu mpya kuajiri

Spread the loveSERIKALI imetangaza nafasi za ajira za watumishi wa umma 46,000...

error: Content is protected !!