Tuesday , 19 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Wadau, wawekezaji watakiwa kutoilalamikia Serikali
Habari MchanganyikoTangulizi

Wadau, wawekezaji watakiwa kutoilalamikia Serikali

Spread the love

SERIKALI imewataka wawekezadi na wadau mbalimbali kuachana na tabia ya kulalamika serikali na badala yake watoe ushauri kwa serikali ni jinsi gani ya kutatua changamoto mbalimbali. Anaripoti Dany Tibason … (endelea).

Kauli hiyo ilitolewa na Waziri wa Biashara Viwanda na Uwekezaji, Charles Mwijage.

Mwijage alitoa kauli alipokuwa akifungua mkutano wa wadau na wawekezaji wa pamba, bidhaa za nguo na mavazi katika ukumbi wa mikutano wa Hazina mjini hapa.

Amesema pamoja na kuwepo kwa changamoto mbalimbali zinazokabiliana na wizara hiyo lakini ni wakati wa wadau kutoa maoni yao ya kuishauri serikali pamoja na kuisaidia ili iweze kufanikiwa badala ya kuendelea kulalamika.

Hata hivyo amesema kwa kuzingatia kuwepo kwa sera ya serikali ya viwanda ni wakati sasa wa waekezaji kujenga viwanda ambavyo vitaweza kuzalisha malighafi ambazo zinazalishwa nchii badala ya kuuza nje na kununua bidhaa zinazozalishwa nje ya nchi.

Akizungumzia zao la pamba amesema kwa kuwa wananchi na wakulima wamehamasishwa zaidi kulima pamba katika maeneo ya ukanda wa pamba ni lazima pamba inayozalishwa nchini isiuzwe nje ya nchi na badala yake ichakatwe na kuzalisha nguo na nyuzi ambazo zinaweza kutumiwa na kuzalisha bidhaa bora.

Kwa upande wake mkuu wa Wilaya ya Gairo Mkoani Morogoro, Siriel Mchembe, ameitaka serikali kuhakikisha inaweka mikakati ambayo inaeleweka kwa lengo la kujua soko la pamba pamoja na bei ambayo itakuwa inamanufaa kwa wakulima.

Akichangia katika mkutano huo mkuu huyo wa wilaya ambaye alikuwa amemwakilisha mkoa wa Morogoro, amesema kwa sasa wananchi wamehamasishwa zaidi kulima zao la pamba na kufikia hatua ya kuachana na kilimo cha mahindi hivyo wanatakiwa kuhakikishiwa kama pamba yao itakuwa na soko la uhakika.

“Kwa sasa wakulima wamehamasishwa sana kulima pamba imefikia hatua wapo wakulima ambao wameachana na kulima mahindi wakijua kuwa pamba itakuwa na bei nzuri, sasa ikitokea pamba ikaa haina soko au kuonekna ni chafu je wakulima hao tutawaambia nini,” alihoji mkuu huyo wa wilaya.

Naye mkuu wa mkoa wa Mara, Adam Kigoma Malima amesema haiweze, mawaziri, wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya pamoja na wetendaji wengine wakaishi kwa kulalamika badala ya kutafuta suluhusho.

Amesema suala la uwepo wa viwanda unatakiwa kuwa na mikakati ya pamoja nadala ya kuishi kwa malalamiko na kukosa ufumbuzi na maazimio ya pamoja na kwa hali hiyo haiwezekani pakawepo na maendeleo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Diwani, wananchi wengine 463 wahama Ngorongoro

Spread the loveMakamu mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Ngorongoro ambaye pia...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Shule zafungwa kutokana na ongezeko la joto

Spread the loveSUDAN Kusini imeamuru kufungwa kwa shule zote kuanzia leo Jumatatu,...

Habari Mchanganyiko

Bunge laja na Marathon kuchangia ujenzi wa sekondari

Spread the loveBUNGE la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linatarajia kukusanya fedha...

error: Content is protected !!