Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Wadau wa elimu waililia serikali mtaala wa elimu
Elimu

Wadau wa elimu waililia serikali mtaala wa elimu

Prof. Joyce Ndalichako, Waziri wa Elimu
Spread the love

WADAU wa elimu nchini wamehoji walimu kutoshirikishwa katika mchakato wa kuandaa mtaala wa elimu mwaka 2016, kabla ya serikali kuupeleka mashuleni. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Wakichangia katika mada iliyohusu mtazamo wa walimu kuhusu Mtaala wa elimu wa mwaka 2016, wadau hao walihoji ni kwanini umekuwa na sintofahamu nyingi huku wakitaka kujua ni kwanini  haukuwashirikisha walimu kabla ya Serikali kuupeleka mashuleni.

Wadau hao walikuwa katika mkutano wa siku tatu uliandaliwa na  Mtandao wa Elimu Tanzania Ten/Met kujadili ubora wa elimu nchini.

Akiwasilisha mada hiyo, Mshauri wa Elimu kutoka Haki Elimu, Wildaforce Maina, alisema katika utafiti alioufanya mwaka 2018, amegundua kwamba walimu wengi hawana uelewa kuhusiana na mtaala wa elimu wa mwaka 2016.

“Nilifanya utafiti wangu mwaka 2018 na nilichogundua ni kwamba walimu wengi hawana uelewa kuhusiana na mtaala wa mwaka 2016 wengi wameukuta wakati wa kufundisha tu hawajui ukoje hivyo wamekuwa wakifundisha tu bora liende,” alisema.

Mshauri huyo wa elimu aliishauri Serikali kuwashirikisha walimu pindi ambapo kunakuwa na mabadiliko ya mitaala ili iwe rahisi kujua changamoto zipi ambazo zipo kwa walimu pamoja na wanafunzi.

Kwa upande wake, Meneja Program, kutoka Chama cha Wamiliki wa Shule Binafsi Tanzania (TAPIE), Laurent Gama alisema mtaala wa elimu wa mwaka 2016 ulitangulia darasani kabla ya walimu hawajaujua unataka nini.

“Rai yangu mabadiliko lazima yaendane na mahitaji lazima kuwe na vifaa vya utekelezaji, vifaa visichelewe kama ambayo mtaala unataka, lazima kuwe na usimamizi mzuri, lazima kuwe na vitabu, lakini ni lazima walimu wapate mafunzo,” alisema.

Naye, Mtaalamu wa elimu kutoka Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Peter Mlimahadala alisema mitaala walimu kutoijua mapema inaathari kubwa kwa taifa kwani wanafunzi wanaozalishwa wanakuwa hawana  ubora unaotakiwa.

“Walimu wao ndio wanaweza kueleza changamoto kwa sababu ndio wanaofundisha wao ndio wanatakiwa kutoa ushauri tunatakiwa tufundishaje, hili ni muhimu sana kwa taifa letu baadae tutakuwa na wataalamu ambao ni jina tu,” alisema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanawake GGML wawanoa wanafunzi Kalangalala Sec. kujitambua

Spread the loveKATIKA kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani, Umoja wa...

ElimuHabari Mchanganyiko

RC Songwe ang’aka kesi 2 kati ya 60 za mafataki kuamuliwa

Spread the loveMkuu wa mkoa wa Songwe Dk. Fransis Michael ameshangazwa na...

error: Content is protected !!