Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wadaiwa pango la ardhi kukiona
Habari Mchanganyiko

Wadaiwa pango la ardhi kukiona

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi 
Spread the love

WATU wanaomiliki ardhi mijini, mashambani na vijijini, wametakiwa kulipa kodi ya ardhi kabla ya Januari 2021, vinginevyo watafikishwa kortini. Anaripoti Regina mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Willium Lukuvi, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ametoa wito huo wakati akizungumza na Shirika la Utangazaji la Tanzania (TBC), kwenye kipindi cha Ardhio.

Amesema, watu hao wanatakiwa kulipa kwa hiyari na kwamba, wakishindwa kufanya hivyo, watafikishwa mahakamani na kulazimika kulipa na faini.

“Ujumbe wangu wa mwisho kwa mwaka huu, ni kwa wamiliki wote wenye hati za ardhi mijini na mashambani, wanatakiwa kulipa kodi ya ardhi kwa hiyari, mwakani watalazimika kulipa kodi na faini,” amesema.

Kwenye kipindi hicho, Lukuvi amehimiza wanafamilia kumiliki ardhi kwa pamoja kwa mujibu wa sheria ya 1999, ili kupunguza migogoro pale wanapotengana ama mmoja kutangulia mbele ya haki.

Amesema, amekutana na migogoro mingi kuhusu watu kudhulumiana ama kutengana ama mmoja kufariki, ambapo amesisitiza matumizi ya sheria hiyo ni mwarobaini wa migogoro ya ardhi katika umiliki wake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Gardner Habash wa Clouds Fm afariki dunia

Spread the loveALIYEKUWA mtangazaji wa kipindi cha Jahazi kinachorushwa na kituo cha...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

error: Content is protected !!