Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Wachimbaji madini wanawake wamlilia Magufuli 
Habari Mchanganyiko

Wachimbaji madini wanawake wamlilia Magufuli 

Spread the love

WACHIMBAJI madini wanawake nchini wameitaka serikali kuwawezesha ili kukuza sekta hiyo inayochangia pato la taifa na kukuza ajira kwa vijana, anaandika Pendo Omary.

Kauli hiyo imetolewa wakati wa warsha ya upatikanaji wa rasilimali zalishi- sekta za ardhi, madini na kilimo zilizofanyika wakati wa tamasha la jinsia la 14 ambalo limeandaliwa na asazi za kiraia, wanaharakati ngazi za jamii na kuratibiwa na TGNP- Mtandao.

Rachel Joseph, Mwenyekiti wa Chama cha Wachimbaji Madini Wanawake nchini (TAWOMA) ameuambia mtandao wa MwanaHALISI Online  anataka Rais Magufuli awasikie.

Amesema hakuna wanayeshindana naye duniani katika kuchimba madini ya Tanzanite na kwamba wanatakiwa kuchimba kidogokidogo wao  wenyewe.

Amehauri kuwa kwa sasa hakuna  haja ya kuleta wawekezaji kutoka nje, inachopaswa serikali ni kutuwezesha kwa kutupatia ruzuku ili wachimbe kisasa.

Rachel ambaye pia ni kati ya wanawake 30 wanaochimba madini ya Tanzanite Melelani amesema wanawake wachimbaji wanakabiliwa na chanagamoto zaidi kuliko wanaume hivyo wale wanaoweza vizuri kazi hiyo wanapaswa kuwezeshwa ili kuwachochea watoto wa kike kujiajili katika sekta hiyo ili kupunguza tatizo la ajira.

Aidha,   kwa upande wake Sarah Lusambagula, mvumbuzi wa madini ya kombati amesema suala la kupata vibali vya kuendesha shughuli hizo limekuwa ni changamoto.

“Tunapogundua maeneo yenye madini mara baada ya kufanya tafiti, tunalazika kuomba vibali serikalini, lakini tunachokumbana nacho huko ni rushwa na pale unaposhidwa kuwapatia lile eneo uliloligundua anapewa mtu mwingine licha ya kwamba ulikuwa na vigezo vya kupata leseni,” anasema Sara kutoka Wilaya ya Ludewa mkoa wa Njombe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

Habari Mchanganyiko

NMB yafuturisha Dar, Majaliwa azitaka Serikali za Mitaa, Taasisi zijifunze kwao

Spread the loveBENKI ya NMB imewafuturisha wateja wake walio kwenye Mfungo wa...

error: Content is protected !!