Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wachafukoga marufuku kuingia mjini-Makonda
Habari Mchanganyiko

Wachafukoga marufuku kuingia mjini-Makonda

Spread the love

WATANZANI wachafu wamepigwa marufuku kuonekana mijini hususani katika kipindi hiki cha Mkutano wa Nchi Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC). Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Marufuku hiyo imetolewa na Paul Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam leo tarehe 29 Julai 2019, kwenye uzinduzi wa kampeni ya usafi wa jiji hilo.

Kampeni hiyo imezinduliwa ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya mkutano huo wa 39. Mkutano huo unatarajiwa kufanyika kwa siku mbili, kuanzia tarehe 18 hadi 19 Agosti 2019.

Makonda amepiga marufuku ya kuingia katika viunga vya mjini na nguo zisizonyooshwa “tabia ya kuna mjini bila kunyoosha nguo ni marufuku,” na kuongeza “tabia ya kuja mjini hujaoga ni aibu.”

Kiongozi huo wa Dar es Salaam pia ameonya watu wenye tabia za kwenda mjini bila kuwa wasafi, na kwamba ni bora wasubiri mkutano huo upite.

“Watu wanatembea tu na chawa, kama huwezi kuwa msafi basi subiri mwezi huu upite…”kama hufui nguo, kama huogi, pumzika kidogo kuja mjini, kwa kipindi hiki tuvumiliane,” amesema.

Katika kampeni hiyo Makonda ameshauri kwamba, dereva yeyote atakayekamatwa anatupa takataka asitozwe faini na badala yake apewe eneo la kufanya usafi.

Kwenye harakati hizo Makonda amesema, anafanya hivyo kwa kuwa hataki kumtia aibu mkuu wa nchi, Rais John Magufuli ambaye ndiye mwenyeji wa mkutano huo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!