Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Wabunge wateule waitwa Dodoma
Habari za Siasa

Wabunge wateule waitwa Dodoma

Steven Kigaigai, aliyekuwa Katibu wa Bunge
Spread the love

WABUNGE wateule wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wametakiwa kufika Dodoma kwa ajili ya usajili unaoanza leo Jumamosi hadi tarehe 9 Novemba 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Kikao cha kwanza cha Bunge la 12, kitafanyika Jumanne tarehe 10 Novemba 2020 jijini Dodoma.

Katibu wa Bunge, Stephen Kagaigai akizungumza na waandishi wa habari leo Jumamosi tarehe 7 Novemba 2020 ofisi za bungeni, Dodoma amesema, “kikao cha kwanza cha mkutano wa kwanza wa Bunge jipya kitafanyika tarehe 10 Novemba 2020.”

Amesema, usajili na taratibu nyingine za kiutawala zitafanyika ofisi ya Bunge Dodoma.

bunge la tanzania

Kagaigai amesema, wabunge wateule wote wanapaswa kufika wakiwa na nyaraka; hati ya kuchaguliwa/kuteuliwa kuwa mbunge na nakala ya kitambulisho cha Taifa.

Pia, Kadi ya Benki yenye namba  ya akaunti ya mbunge; cheti cha ndoa kinachotambuliwa na Serikali (kwa wenye ndoa), cheti cha kuzaliwa cha watoto wenye umri chini ya miaka 18 (kwa wenye watoto), vyeti vya elimu/taaluma, nakala ya wasifu wa mbunge na picha (pasipoti size) nakala nane.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!