Thursday , 18 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wabunge, wastaafu kuondolewa kwenye nyumba za TBA
Habari Mchanganyiko

Wabunge, wastaafu kuondolewa kwenye nyumba za TBA

Spread the love

WAKALA wa Majengo Tanzania (TBA), wameamua kuondoa wadaiwa sugu katika nyumba zao. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

TBA wameeleza kuwa, wapangaji hao mpaka sasa wamesababisha hasara ya Sh 1.5 Bil na kwamba, miongoni mwa wadaiwa sugu ni wabunge na wastaafu.

Kwa mujibu wa TBA, pia watawaondoa wastaafu kwa kuwa, wanapomaliza utumishi wa umma, wana uwezo wa kuwa na nyumba zao.

 Akizungumza na wanahabari tarehe 20 Agosti 2019, Kaimu Meneja Wakala wa Majengo Mkoa wa Dodoma, Helman Tanguye baada ya kufanya zoezi hilo amesema, wadaiwa hao wamelimbikiza madeni yao kwa miaka 10 sasa.

 Amesema, TBA imekuwa ikidai fedha nyingi na hasa katika Mkoa wa Dodoma kwa wafanyakazi wa serikali na taasisi mbalimbali za serikali ambazo wamezipangisha.

“Mpaka sasa tunadai zaidi ya bil 1.5, hivyo lengo kuu la TBA ni kuwaondoa wale watu walioshindwa kulipa kodi ya pango kwa wakati ili watu wanaohamia kutoka mikoa ya Dar es salaam na maeneo mengine, waweza kupata nafasi ya kupanga katika nyumba hizo,” amesema Tanguye.

Akizungumzia zoezi zima walivyolianza amesema, “tumelianza jana baada ya kufanya taratibu zote za kisheria na mikataba, kwa hiyo tuliwapa notes ya siku 30 badaye tukaongeza Siku 14 lakini zilivyokwisha, tulichukua vyombo ambavyo vinatambulika na mahakama ili tuweze kuwaondoa.”

Amesema, kampuni wanayoitumia katika zoezi zima la kuwatolea watu vitu vyao nje ni Yono Auction Mart ambayo wamekuwa wakiitumia mara kwa mara katika shughuli zao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

Habari Mchanganyiko

Serikali yatoa ajira watumishi 46,000, yatangaza utaratibu mpya kuajiri

Spread the loveSERIKALI imetangaza nafasi za ajira za watumishi wa umma 46,000...

Habari Mchanganyiko

Dereva ajali iliyoua wanafunzi Arusha afikishwa kortini, aomba apelekwe rumande

Spread the loveDEREVA aliyehusika katika ajali la basi la Shule ya Msingi...

error: Content is protected !!