MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam inatarajia kutoa uamuzi wa zuio jipya la kutoapishwa kwa Wabunge wateule wa upande wa Chama cha Wananchi – CUF unaumuunga Mkono Professa Ibrahim Lipumba, anaandika Faki Sosi.
Prof. Lipumba ni mwenyekiti wa CUF anayetambuliwa na ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini.
Leo wakili wa wabunge wa chama hicho waliofukuzwa uanachama na kambi ya Prof. Lipumba, Peter Kibatala mbele ya Jaji Lugani Mwandambo amewasilisha hoja za pingamizi hilo la muda.
“Mahakama kesho itatoa uamuzi wa zuio dogo la muda, juu mapingamizi tuliowasilisha ili wabunge walio ondolewa wabaki kama waliovyo na wale waliotangazwa na tume ya uchaguzi wasiapishwe.
“Tumekubaliana mapingamizi ya awali waliyoleta walalamikiwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali yasikilizwe kwa maandishi na uamuzi juu yake utatoka tarehe 27 Agosti 2017,” amesema.
Mahakama itatoa uamuzi huo kesho saa 7:30 Mchana.
Leave a comment