Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Wabunge wa Chadema wahojiwa Polisi
Habari za Siasa

Wabunge wa Chadema wahojiwa Polisi

Wabunge wa Chadema waliohojiwa kwa tuhuma za kumshambulia Juliana Shonza, Mbunge wa Viti Maalum CCM
Spread the love

BAADA ya wabunge nane wa Chadema kukamatwa na kuachiwa kwa dhamana jana usiku, leo wametakiwa kuripoti Polisi mjini Dodoma kwa mahojiano zaidi, anaandika Hellen Sisya.

Wabunge hao walishikiliwa na Polisi kwa makosa ya kudhuru mwili yaliyoripotiwa na Mbunge wa Viti Maalum CCM, Juliana Shonza muda mchache baada ya pande hizo mbili kulumbana nje ya jengo la Bunge.

Wabunge wa Chadema ambao wanaohojiwa na Polisi ni pamoja na Joseph Selasini, Suzan Kiwanga, Saed Kubenea, Cecilia Pareso,  Francis Mwakajoka na Pauline Gekul.

Sakata hilo lilitokea baada ya wabunge wa Chadema kukutana na Shonza na kumwambia anachikifanya bungeni inatokana na chuki zake na upinzani, hali iliyosababisha naye kujibu mapigo na kuzua mvutano.

Shonza alichangia bungeni alikaririwa akiwasil;isha mapendekezo ya kuongezewa adhabu kwa Mbunge wa Kawe, Halima Mdee kwa lengo la kuendelea kukaa nje ya bunge na ikiwezekana kuongezewa adhabu zaidi.

MwanaHALISI Online itakupa taarifa zaidi kuhusiana na mahojiano hayo yanayoendelea mjini Dodoma.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aridhishwa utendaji mabalozi, awapa neno

Spread the loveRais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza mabalozi  wanaowakilisha ...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the loveMBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze kasi...

error: Content is protected !!