Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Wabunge DRC wamuondoa madarakani Spika  
Kimataifa

Wabunge DRC wamuondoa madarakani Spika  

Felix Tshisekedi, Rais wa DR Congo
Spread the love

BUNGE katika Jamhuri ya Demokrasia ya Watu wa Kongo (DRC), limemuondoa madarakani, aliyekuwa Spika wake, Jeanine Mabunda, kufuatia kupigiwa kura ya kutokuwa na imani naye… Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Hoja ya kumuondoa kwenye kiti chake Spika Mabunda, iliwasilishwa bungeni na wabunge wa upinzani, ambapo kati ya wabunge 484 waliopo katika Bunge hilo, wabunge 281 waliridhia kiongozi huyo, kuachia ngazi.

Ni wabunge 200 pekee waliopinga uamuzi huo, huku chama cha People’s   Party for Reconstruction and Democracy (PPRD), kilichokuwa kikiongozwa na aliyekuwa rais wa nchi hiyo, Joseph Kabila,  kikiwa ndicho chenye  wabunge wengi bungeni.

Inadaiwa kuwa wabunge walichukua uamuzi huo, baada ya kujiridhisha kuwa Spika wao kuendesha Bunge kwa malengo yake ya kisiasa na kutokuwa muwazi kwenye usimamizi wa fedha za Bunge

Kwa mujibu wa taarifa hizo, pendekezo la kumuondoa mamlakani Spika Mabunda, liliwekwa dhidi yake na wafuasi wa rais wa sasa, Felix Tshisekedi, kwa sababu zizizo nje ya kisiasa.

Hata hivyo, Spika Mabunda amekana tuhuma dhidi yake na amewahi kuomba radhi kufuatia kile alichoita, “hali iliyojitokeza ya kutoelewana” na akalisihi Bunge, kukataa pendekezo hilo.

Kupatikana kwa taarifa kuwa Spika Mabuda ameong’olewa mamlakani, kumekuja katika kipindi ambacho kumeibuka madai kuwa uswahiba kati ya Rais Tshisekedi na mtangulizi wake huyo, umeingia doa.

Tshisekedi ambaye aliingia madarakani kupitia muungano wa chama cha Demokrasia na Maendeleo ya Jamii (UDPS), alidaiwa kuwa na uhusiano wa karibu na Rais Kabila, na kuna taarifa kuwa walitengeneza hata “mwafaka wa kuachia madaraka.”

Hata hivyo, kuondolewa kwa spika huyo wa Kongo kunampa rais Tshisekedi ushindi mkubwa katika harakati zake za kuwania madaraka kati yake na wafuasi wa rais mstaafu, Joseph Kabila.

Aliyekuwa mwanachama wa chama cha Kabila, Justin Bitakwira ameeleza kuwa kilichomsababisha Spika Mabunda kung’olewa madarakani, ni hatua ya Rais Kabila, kupuuza maoni ya wengi.

Bitakwira ambaye amepata kuwa waziri katika serikali ya Rais Kabila anasema, shida iliyopo ni kwamba aliyeteuliwa kuwa spika wa Bunge, hakuwa na uwezo wa kushika nafasi hiyo. Anamtuhumu Rais mstaafu Kabila kwa kuwafikisha hapo.

“Shida ya Rais Kabila, anataka kuumba watu. Kwamba, anaweza kuchukua mtu dhaifu na asiyekuwa na uwezo na kumfanya mtu mkubwa sana. Huyu bwana hakuwa na uwezo wa kushika madaraka aliyopewa,” ameeleza.

Anasema, “tabia hiyo ndiyo inayomgharimu Rais Kabila na ndio utakuwa mwisho wake wa kisiasa yeye na  chama chake.”

Katika uchaguzi mkuu wa tarehe 30 Desemba mwaka 2018, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (CENI), ilimtangaza Rais Tshisekedi kuwa mshindi wa kiti cha urais, nyuma ya mgombea mwingine wa upinzani, Martin Fayulu, pamoja na mgombea aliyekuwa anaungwa mkono na serikali, Emmanuel Shadary.

Mkuu wa CENI, Corneille Nangaa, alinukuliwa na vyombo vya habari akisema, Bw. Tshisekedi alipata asilimia 38.57 ya kura zilizopigwa.

Fayulu alipinga matokeo hayo na kusema, “…matokeo haya hayana uhusiano hata kidogo na ukweli halisi. Raia wa Congo hawataukubali utapeli kama huu daima.”

Alisema, “Felix Tshisekedi hakupata kura 7 milioni, hakupata. Alizitoa wapi? Haiwezekani. Hii ni kashfa mbaya sana.”

Aliongeza: “Bw Nangaa (mwenyekiti wa CENI) anafuma kitambaa cheusi kwa uzi wa rangi nyeupe. Nangaa na marafiki zake katika FCC (chama tawala), wamekuwa wakichakachua matokeo kumpa ‘kikaragosi’ wao ushindi.”

Hapo awali, Fayulu alikiambia kituo cha redio cha FFI (Radio France International), kwamba matokeo hayo ni “mapinduzi halisi kupitia uchaguzi,” na akatoa wito kwa waangalizi wa uchaguzi kuchapisha matokeo waliyo nayo aliyosema ni ya kweli.

Lakini Tshisekedi kwa upande wake, alimtaja rais aliyekuwa anaondoka Ikulu – Joseph Desire Kanambe Kabila – kama “mshirika muhimu wa kisiasa.”

Kulikuwa na tetesi kwamba, hata kucheleweshwa kwa shughuli ya kutangaza matokeo, kulilenga kutoa muda kwa Rais Kabila na Tshisekedi kuafikiana.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

KimataifaTangulizi

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the love  TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

error: Content is protected !!