Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kinachonibakisha CUF si Prof. Lipumba-Mbunge CUF
Habari za Siasa

Kinachonibakisha CUF si Prof. Lipumba-Mbunge CUF

Hamidu Bobali, Mbunge wa Mchinga
Spread the love

HAMIDU Bobali, Mbunge wa Jimbo la Mchinga, Lindi amesema kuwa, hatoacha ubunge na kujiunga ACT-Wazalendo alikohamia Maalim Seif Sharif Hamad, aliyekuwa Katibu Mkuu wa CUF. Anaripoti Regina Mkonde…(endelea).

Amesema, hatofanya hivyo kwa sababu hatua hiyo inaweza kusababisha taifa kuingia kwenye hasara ya kurudia uchaguzi na kupoteza fedha nyingi lakini pia hawezi kujizulu kwani atakuwa amesaliti walimpigia kura wake.

Akizungmza leo tarehe 19 Machi 2019 Bobali amesema kuwa, hajabaki CUF kuungana na Prof. Lipumba ili kulinda ubunge wake, bali amechukua hatua hiyo kwa ajili ya kulinda masilahi ya wapiga kura wake na kuokoa fedha za umma.

“…muda wa kwenda mahakamani haupo, tuachane na habari za kesi turudi kujenga chama chetu,” amesema Bobali nakuongeza; “Natoa rai kwa wabunge wenzangu, madiwani na wenyeviti tusikimbie chama chetu, tuje tujenge chama chetu.”

Katika hatua nyingine, Bobali ameomba radhi uongozi wa CUF na yeyote aliyemkosea ndani ya chama hicho. “Na leo ninautangazia umma na chama, nikiwa mbunge na mwanachama naamini yule niliyomkosea, mwenyekiti atakuwa amenisamehe. Ninachukua fursa hii kuomba radhi wanachama wote na viongozi wa CUF ambao kwa namna moja au nyingine tumekosena.’

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!