SPIKA wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai amewapisha wabunge 19 wa viti maalum kupitia Chama cha Demokraisa (Chadema). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).
Spika Ndugai amewaapisha leo Jumanne tarehe 24 Novemba 2020 viwanja vya Bunge jijini Dodoma
Walioapishwa ni; Halima Mdee, Grace Tendeka, Esther Matiko, Cecilia Pareso, Ester Bulaya, Agnesta Lambat, Nusrat Hanje, Jesca Kishoa, Hawa Mwaifunga na Tunza Malapo.
Wengine ni; Asia Mwadini Mohamed, Felister Njau, Naghenjwa Kaboyoka, Sophia Mwakagenda, Kunti Majala, Stella Siyao, Salome Makamba, Anatropia Theonest na Conchesta Lwamlaza.
Kati ya wabunge hao 19 walioapishwa, wanaoingia kwa mara ya kwanza ni wanne; Agnesta, Asia, Stella na Felister.
Nadhani hiki ni kipindi cha chadema kupasuka, kwani mgawanyiko huu hauna afya