Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Waandamanaji wamiminiwa risasi za moto Nigeria
Kimataifa

Waandamanaji wamiminiwa risasi za moto Nigeria

Spread the love

NCHINI Nigeria, zaidi ya miili 20 imepatikana baada ya kumiminiwa risasi na jeshi la nchi hiyo kuwamiminia risasi waandamanaji wanaopinga ukatili wa polisi nchini humo. Inaripoti mitandao ya kimataifa…(endelea).

Taarifa kutoka mashirika mbalimbali ya habari yanaeleza, watu zaidi ya 50 wamejeruhiwa wakati wanajeshi wakimimina risasi waandamanaji hao katika viunga kwa Lagos, Nigeria.

Mauaji hayo yamefanyika jana jioni Jumanne tarehe 20 Oktoba 2020, Lagos na wanaotajwa kuwa wanajeshi wa taifa hilo waliovalia kiraia.

Askari wenye silaha walikuwa wakiwazuia waandamanaji kabla ya risasi kuanza kurindima.

“Walikuwa wanapiga risasi moja kwa moja kwetu, lilikuwa tukio baya. Kuna mtu alipigwa risasi na kufa hapo hapo.

“Walipiga risasi kwa muda wa saa moja na nusu na baada ya hapo, askari walichukua miili ya waliouawa,” shuhuda mmoja aliiambia BBC.

Askari walikuwa wameweka zuio kwa waandamanaji, hivyo magari ya wagonjwa yalishindwa kufika katika eneo la maandamano.

Shirika la kimataifa la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limeeza kupata habari za kuaminika kuhusu vifo hivyo.

Taarifa ya Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC) zimeeleza, maofisa wa jeshi Nigeria wameahidi kufanya uchunguzi kuhusu shambulio hilo.

Katika Jiji la Lagos na maeneo mengine, wananchi wamepewa amri ya kutotoka nje. hata hivyo, waandamanaji wameendelea kujitokeza na kuzingira vituo vya polisi.

Kutokana na mapigano ya risasi yanayoendelea , Hillary Clinton, aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje Marekani amemtaka Rais wa Nigeria, Muhammadu Buhari kuacha kuua vijana.

Odion Jude Ighalo, mcheza wa Manchester United, kupitia ukursa wake wa twitter ameishutumu Serikali ya Nigeria kwa kuua wananchi wake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!