Tuesday , 23 April 2024
Home Habari Mchanganyiko ‘Vyombo vya haki viboreshwe, mahabusu wapone’
Habari Mchanganyiko

‘Vyombo vya haki viboreshwe, mahabusu wapone’

Spread the love

FAMILIA tatu mkoani Mtwara zimeiomba Serikali ya Tanzania, kuboresha utendaji wa vyombo vyenye dhamana ya kutoa haki, ili kuondoa changamoto ya watuhumiwa kukaa mahabusu muda mrefu, kwa madai ya upelelezi wa makosa yao kutokamilika. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Ombi hilo limetolewa leo Alhamisi tarehe 9 Julai 2020, jijini Dar es Salaam na Tiba Moshi Kasoko kwa niaba ya familia hizo tatu.

Familia hizo zimetoa ombi hilo baada ya ndugu zao, Omar Salum Bumbo (51), Ustadhi Ramadhan Moshi Kasoko(41) na Waziri Suleiman Mkaliganda (33) kusota mahabusu kwa zaidi ya miaka miwili katika Mahabusu ya Gereza la Lilungu mkoani Mtwara kwa madai ya kutokamilika kwa ushahidi wa makosa yao.

Watatu hao walikamatwa katika nyakati tofauti mwaka 2017, ambapo wanakabiliwa na tuhuma za makosa ya ugaidi, katika Mahakama ya Wilaya ya Mtwara.

Akizungumza kwa niaba ya familia hizo, Kasoko ameziomba mamlaka husika kukamilisha taratibu za kisheria ili watuhumiwa hao na wengine walioko mahabusu, mashauri yao yatolewe uamuzi, ili kama wana hatia wafungwe au kama hawana hatia waachwe huru.

“Tunaiomba Serikali ya wanyonge inayosimamia haki ili ndugu zetu na mahabusu wengine mfano wao ambao wanaendelea kukata miaka mahabusu watekelezewe kwa haraka utaratibu wa kisheria ambao ni haki yao,” amesema Kasoko na kuongeza:

“Ili kesi zao zisikilizwe na kama ushahidi haujakamilika wapatiwe dhamana na kama haupo waachiwe huru, kuliko kubaki katika hali ya sasa ambayo inatoa sura ya wazi ya uonevu.”

Hata hivyo, Kakoso amesema suala hilo amelifikisha katika Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP), ambayo ilikiri kupokea faili la watuhumiwa hao, na kuahidi kulifanyia kazi.

” Kabla ya kuzungumza na ninyi wanahabari niliwahi kufika Dodoma kwa DPP, akasema mafaili yao yako kwake akasema yatashughulikiwa,” amesema Kakoso.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Watuhumiwa 12 wa kilo 726.2 za dawa za kulevya wafikishwa mahakamani

Spread the love  WATUHUMIWA watatu wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kibaha Mkoani...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari Mchanganyiko

GGML yasisitiza kuendelea kuimarisha afya za wafanyakazi

Spread the loveKAMPUNI ya Geita Gold Mining Limited kwa kushirikiana na kampuni...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

error: Content is protected !!