Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Viti maalum: Spika Ndugai awashangaa Chadema kulumbana
Habari za Siasa

Viti maalum: Spika Ndugai awashangaa Chadema kulumbana

Spika Job Ndugai
Spread the love

SPIKA wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai ‘amekishangaa’ Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kuendelea na mjadala wa ama wapeleke majina ya wabunge wa viti maalum bungeni au wasipeleke. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Ndugai ametoa maelezo hayo bungeni leo Alhamisi tarehe 12 Novemba 2020, kabla ya kuahirisha shughuli za Bunge mchana jijini Dodoma akisema, bungeni kuna wabunge wa aina nne.

Amesema, kuna wabunge wa majimbo, nafasi tano za Baraza la Wawakilishi, nafasi kumi za Rais ambazo huteua anayemtaka na wale wa viti maalum.

Spika Ndugai amesema, nafasi za wajumbe wa Baraza la Wawakilishi zitapatikana katika mkutano wa Bunge unaokuja lakini “Kuna vyama bado havijaleta wabunge hasa wa viti maalum, tunachoona mitandaoni huko wanalumbana, eti walete, wasilete.”

“Kwa sababu ni fursa za kina mama wanalumbana, ingekuwa za wanaume, wangekuwa wamefika hapa. Haipaswi kuwa hata mjadala,” amesema Spika Ndugai.

Akiendelea kueleza, Spika Ndugai amesema “wapiga kura wengi kina mama unawazuiaje, wewe unazuiaje, haipaswi kuwa hata mjadala. Iko fursa hupaswi kuichezea.”

Halima Mdee

Katika matokeo ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 28 Oktoba 2020, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) ilinukuliwa ikisema, vyama viwili vya CCM na Chadema ndivyo vyenye sifa ya kupata wabunge wa viti maalum.

CCM imejipatia viti maalum 94 huku Chadema ikipata 19.

Hata hivyo, viongozi wakuu wa Chadema pamoja na ACT-Wazalendo, walijitokeza mbele ya waandishi wa habari na kupinga matokeo ya uchaguzi huo kwa madai uligubikwa na ukiukwaji wa sheria, kanuni na miongozo.

Vyama hivyo, vilitaka uitishwe upya uchaguzi mkuu na usimamiwe na Tume Huru ya Uchaguzi upande wa Tanzania bara na Zanzibar huku ukiitosha maandamano ya amani yasiyokuwa na kikomo kuanzia tarehe 2 Novemba 2020.

Hata hovyo, maandamano hayo hayakufanyika na kujikuta baadhi ya viongozi wake wakishikiliwa na polisi kwa siku kadhaa kisha kuachiwa na wanaendelea kuripoti polisi kwenye maeneo mbalimbali nchini.

Kutokana na hali hiyo, ndani na nje ya Chadema, kumekuwa na mjadala mkali wa ama wateue wabunge wa viti maalum au waachane navyo.

Kumekuwa na hoja mbili, ikiwamo kwamba, wakiteua wa kuwapeleka bungeni, itakuwa wanakubaliana na matokeo ya uchaguzi waliyosema haukuwa huru na haki na wengine wanasema, wasiende kwa kuwa haukuwa uchaguzi huru na haki.

Tundu Lissu, aliyekuwa mgombea urais wa Tanzania kupitia Chadema katika uchaguzi huo, ni miongoni viongozi wa Chadema ambao wamejitokeza hadharani kupinga kupeleka wabunge wa viti maalum.

“Kupekela wabunge wa viti maalum ni kuhalalisha uchafuzi wa uchaguzi uliofanyika. Hivyo msimamo wa chama wa kamati kuu ni kutopeleka wabunge wa viti maalum,” alisema Lissu ambaye pia ni makamu mwenyekiti wa chama hicho (bara).

4 Comments

  • CHADEMA isipokonye wanawake haki hao ya kikatiba kupitia viti maalum, ingelikuwa wanaume pangechimbika Leo wanawake 19 wote wanagomewa na uongozi kwa mabavu ili hali hao viongozi akina mnyika na mbowe walishakaa Bungeni na kulipwa mafao yao, HATUONI SABABU

  • Maamuzi ya Chama hufanywa na Mkutano mkuu wa Chama, sasa Huyo Lissu yeye nani hata akatae matakwa ya kikatiba ya nafasi ya viti maalum, kama sio Udikteta.

  • Mpiganaji kamwe hali makombo. CHADEMA si chama masihara kulamba lamba ukoko kwenye mwiko. Kampeni tumeziona na waliozidiwa mpaka wakaanza kuiga sera tuliwaona je kigezo cha ushindi wa halali ni nini kama siyo watu kugongwa kisera hadi wakapiga magoti. Vituoni masanduku yalijazaa ingawa misitari ya wapiga kura haina watu. Thamani ya msimamo wa kukataa viti maalumu utaonekana 2025. Katiba inataka vyama vishindane kwa hoja ili kupata ushindi wa kweli. Kupora ushindi halafu ukawazoba uliowanyang’nya haki ya kupata wabunge kwenye uwanja wa mashindano kwa wabunge wa viti maalumu ni haramu.HOJA YA VITI MAALUMU BILA WABUNGE WAPIGANAJI NI MFU. NAOMBA HIVYO VITI 19 VIENDE CCM MAANA WANA 100% YA WABUNGE WA MAJIMBO.

  • Ngungai alitamka wazi hukutakua na upinzani bungeni bunge la 2025 sasa hao maalum wa nn na wenyewe walioshinda wamepokonywa haki zao kwa mabavu ya wanausalama kama vita! Aceelewa mjinga na mijanga usimpe maana acha abak na ujinga wake

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!