Wednesday , 24 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Vita dhidi ya Corona: Wanywa bia baa wapigwa ‘stop’
Habari Mchanganyiko

Vita dhidi ya Corona: Wanywa bia baa wapigwa ‘stop’

Spread the love

SOPHIA Mjema, Mkuu wa Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam, amepiga marufuku mikusanyiko ya watu katika baa, ikiwa ni sehemu ya hatua za kudhibiti maambukizi ya Ugonjwa wa Homa Kali ya Mapafu inayosababishwa na Virusi vya Corona (COVID-19). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Mjema ametoa marufuku hiyo jana tarehe 17 Aprili 2020, na kuelekeza wamiliki wa baa hizo kuhakikisha wateja wao wanaonunua bia, wanakwenda kunywea nyumbani.

Mjema amesema mtu yeyote atakaye kiuka agizo hilo atachukuliwa hatua za kisheria.

“Waendesha baa mnaelekezwa kuwa vinywaji vitauzwa na mnunuzi atapaswa kunywea nyumbani, na sio kwenye baa. Ni wajibu wa kila mmoja kuzingatia maelekezo haya kwani hatua za kisheria zitachukuliwa kwa mmiliki, muendeshaji na mtu yeyote atakaye onekana kwenye eneo la baa akiendelea kunywa,” amesema Mjema.

Jiji la Dar es Salaam linaongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya maambukizi ya COVID-19, ikifuatiwa na Zanzibar.

Kwa mujibu wa taarifa ya Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya, jiji hilo lina wagonjwa wapya 38 kati ya wagonjwa 53 walioripotiwa jana katika mikoa saba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

error: Content is protected !!