Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya Visa vipya 14 vya Corona vyaripotiwa Tanzania
AfyaHabari MchanganyikoTangulizi

Visa vipya 14 vya Corona vyaripotiwa Tanzania

Spread the love

SERIKALI imetangaza ongezeko la  “kesi mpya kumi na nne” (14) za maambukizi ya ugonjwa wa Corona (Covid 19) nchini. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaaam … (endelea).

Taarifa ya wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, iliyosainiwa na waziri wa wizara hiyo, Ummy Mwalimu, imeeleza kuwa wagonjwa wote wapya, ni Watanzania.

“Wizara inatoa taarifa kuwa kuna ongezeko la wagonjwa wapya 14 kutoka 32 waliokuwapo awali,” ameeleza Waziri Ummy na kuongeza, “kati ya hawa wagonjwa 13 wamepatikana Dar es Salaam na mmoja jijini Arusha.”

Amedai kuwa wagonjwa wote hao wanaendelea na matibabu chini ya uangalizi wa wataalam wa afya.

Amesema, serikali inaendelea kufuatilia watu waliokaribu na wagonjwa hao na kwamba serikali inaendelea kuwataka wananchi kuepuka misongamano.

Hii ni mara ya kwanza kwa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kuripoti idadi kubwa ya wagonjwa wa Corona kwa mara moja, tangu kuibuka kwa ugonjwa huo takribani mwezi mmoja uliyopita.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Gardner Habash wa Clouds Fm afariki dunia

Spread the loveALIYEKUWA mtangazaji wa kipindi cha Jahazi kinachorushwa na kituo cha...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

error: Content is protected !!