Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Vipaji vya watoto kusakwa Leaders Club
Habari MchanganyikoMichezo

Vipaji vya watoto kusakwa Leaders Club

Spread the love

KAMPUNI ya kuandaa filamu nchini Tanzania (J FILM 4 LIFE), imeanza utaratibu wa kutafuta vipaji vya kuigiza kwa watoto ili kushiriki kwenye vilamu mpya ya watoto wanayotarajia kuiandaa. Anaripoti Martin Kamote….(enedelea).

Akizungumza na wanahabari leo tarehe 2 Septemba 2019, mmiliki wa kamopuni hiyo, Jenifer Kyaka ambaye ni maarufu kwa jina la Odama amesema, kampuni hiyo mpaka sasa imeweza kutengeneza filamu zaidi ya 21  na tanthilia.

“Leo ni siku muhimu sana katika sekta ya tasnia yetu ya filamu hasa kwa watoto hapa nchini Tanzania kwasababu, nazindua rasmi mchakato wenye lengo la kutafuta na kuvumbua watoto wenye vipaji vya kuigiza katika tamthilia.

“Watakaochaguliwa, nitawashirikisha katika tamthilia mpya ya watoto inayokuja kuandaliwa na kampuni,” amesema.

Pia amesema, pamoja na ukuaji wa tasnia ya filamu nchini, pia kumekua na changamoto mbalimbali katika soko na tasnia kwa ujumla wake.

Na kwamba, miongoni mwa changamoto ni kutokuwepo kwa mifumo na njia za uhakika katika uuzaji na usambazaji wa filamu, hivyo kupelekea soko kuanza kuhama kutoka katika filamu kuelekea kwenye tamthilia.

https://youtu.be/Q3G_Q8hpq90

Amesema, JFILM 4 LIFE imeamua kuanza mchakato wa  kuandaa tamthiliya kubwa inayolenga watoto, ikielezea zaidi maisha yao katika mambo mbalimbali.

“Miongoni mwa mambo katika tamthilia hiyo ni pamoja na elimu, afya,  migogoro ya familia kwa watoto, dini, mirathi, tamaduni na mila,unyanyasaji wa watoto na ubakwaji,” amesema.

Kazi ya kupata watoto wenye vipaji  vya kuigiza itafanyika Jumamosi tarehe 14/09/2019 saa 3 kamili asubuhi katika viwanja vya Leaders Club kuanzia saa tatu kamili asubuhi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

Michezo

Tusua mkwanja na mechi za Ijumaa leo

Spread the love  LEO hii mechi zinaendelea kote na wewe kama unataka...

error: Content is protected !!